Sunday, November 27, 2016

NAKUPENDA NASRA

MTUNZI:ZUBERI MARUMA

MWANZO

UTANGULIZI

Mapenzi ni hisia kamilifu zitokazo ndani ya moyo wa mwanadamu,nimekukabidhi hisia zangu kwa kuwa umejitoa kwa ajili yangu kwa kunikabidhi moyo wako

Kwa nini nisikupende NASRA?!

Mengi  magumu tumeyapitia yalohatarisha maisha yetu,yote ni kulinda penzi letu

Hivyo vyote ndivyo  vilivyo ongeza ladha maridhawa ya kukupenda

NAKUPENDA NASRA.....

                     **********
GODNAND ni kijana wa kwanza katika familia ya watoto wawili.

anaishi yeye na mdogo wake aitwaye DICK
Katika nyumba ya mama yao aliyefariki kwa ajali ya gari ,wakati akitoka kazini,

baada ya mazishi kuisha kikawekwa kikao cha ukoo .kikao cha familia

Kikao ambacho kilipendekeza mashamba na nyumba yarithiwe na mjomba.Ambaye atachukua jukumu la kuwalea watoto(GOD na DICK)

Ikabidi mjomba ake GOD ALEX akiwa na mke wake MERY na mtoto wao MERINE waje waishi katika nyumba ya marehemu dada  yao

Baada ya siku kadhaa MERY mke wa mjomba ake GOD akaanza manyanyaso kwa kina GOD
Na DICK  akiwanyima chakula,

Ikabidi GOD atafute vibarua mtahani ili hapate ela ale yeye na mdogo ake.

Siku moja  GOD alirudi nyumbani na kumkuta MERINE mtoto wa mjomba ake anakata mkungu wa ndizi shambani,

god analeta shida na kumpiga,

Merine huku akilia anaenda kusema kwamama yake

MERY anakuja huku hasira zikiwa zimempanda,na kuanza kumtukana GOD Ugomvi mkubwa unazuka,

Wakirushiana maneno majirani wanakuja kuwahamua

ALEX mjomba ake GOD baada ya kutoka kwenye miangaiko anamkuta mkewe kafura kwa hasira,

anamuuliza tatizo mery anamwambia juu ya kubadilika kwa GOD

ALEX anamwita GOD na kumuuliza sababu ya kugombana na mke wake.

"Sikilizaiza nkwambie mjomba mimi ni mtu mzima na si mtoto kama udhaniavyo na haki ya kuangalia mali ya wazazi wangu,sitokubali nione icho kimdoli chako kikiharibu ndizi zangu nami nikiwemo,

"mjomba: "eti nini?"

Huku bumbuwazi likiusoma uso wake

god: "sirudii mim nnachoitaji ni hati ya mashamba na nyumba hizi ni mali za wazazi wang naitaji niziongoze mwenyewe

"mjomba: "god unadharau koo,mila na desturi siyo?"

god: (huku akiwa na hasira) "akuna cha ukoo,wala mila amtaishi kwa amani nyinyi bila kunikabidh mali za marehemu mama yangu sawa?"

Alimalizia GOD na kuondoka! ,akimwacha mjomba wake ktk hali ya sintoamini

"dah huyu mtoto sasa ananipanda hadi kichwani ngoja sasa ntamwonesha,ni mdogo tu awezi nizidi mimi akili"

MUHANGA

riwaya : Muhanga
What,sup: 0746206428
Cover: SIMULIZIMAHIRI.BLOGSPOT.COM
     

       LIBERIA  GBARNG

Yowe kubwa lilisikika na kusababisha magwi mkubwa katika jengo moja la jeshi liliopo mji wa Gbarng ndani ya nchi ya Liberia huku sauti za watu zenye rafudhi ya ki liberia zikifoka na kuendelea kumtesa mtu alie endeleza kupiga mayowe huku matusi ya kiswahili yakimtoka bila mpangilio.
kama  ni wewe msomaji ungesikia yowe lile na matusi yale ungeweza kujua aliekuwa akiteswa waliberia wale alikuwa ni mtanzania halisi!
"muachenini muda wake wakuteswa vizuri bado hujafika mfungeni tukamuite boss" mliberia mmoja alie valia nguo za jeshi la liberia aliongea na mwanajeshi mwingine akachukua kamba na kumkalisha kwenye kiti mtanzania alie tapakaa damu na majeraha kadhaa kwenye mwili wake ambayo kwa hakika yalikuwa ni majeraha ya risasi.
mwenajeshi yule alimfunga mtu yule ambaye bila shaka alikuwa ni mateka wao ,alimfunga ki ustadi kwenye kiti kile alipo maliza kumfunga akampiga ngumi nzito ya kifua  mguno wa maumivu ukamtoka mtanzania.
"tayari tuondokeni tusije kumua kabla ya boss kufika" alisema

Baada ya kuachwa kwa muda akiwa kwenye kiti kafungwa kwaustadi mkubwa  kwenye kichwachake kikiwa kimeinamia moja kwa moja kifuani pake ambapo pametapaa damu na kufanya tshirt aliyo ivaa iogepeshe kuitazama , alikuwa kimya wala mwili wake haukutikisika ungeweza kusema amekufa . akili na mawazo yake havikuwa eneo lile alicho fikiria ilikuwavni jinsi ya kujikoa kutoka mahabusu ile mahabusu iliyo jaa kila dalili za umauti. mawazo yake yalikatishwa na sauti ya hatua za watu walio kuwa  kwenye kolido wakija chumba alicho kuwa yeye
"they coming"  alijisemea moyoni huku presha yake ikipanda kwani alikuwa anajua kilicho kuwa kina fuata .alitulia vile vile kichwa chake kikiwa bado kime angukia kifuani .
alisikia sauti ngeni ya kijeshi ikiamulu kwa lugha iliofanana na kiarabu  na hapo akasikia kufuri la chumba likifunguliwa  akili yake ikampa kuwa askali walikuwa wamekuja na mkubwa wao . hakujitikisa wala kuinua kichwa na mara alihisi wapo mbele yake
"ame kufa..." mwanajeshi wa ki liberia aliuliza kwa lugha yao
mmoja wa maaskali  alichukua ndoo yenye maji na kummwagia 
"ni mzima afande huyu ..." alisema askali alie kua kavalia tishirt ya kijeshi na  suruale yake, kisha akaitupa ile ndoo pembeni .
kisha yule mwanajeshi alieonekana kuwa mkubwa alipiga hatua na kuvuta kiti kingine na kukaa mbele ya mateka wao na kumkabili sawa sawa uso kwa uso  kisha akawapa ishara wamtoe kile kitambaa cheusi usoni .
askari mmoja akasogea na kukitoa kile kitambaa na hapo macho manne yalitazamana sambamba baina ya  mateka huyu mtanzania na mwanajeshi wa ki liberia kwa sekunde mbili..
"now you see the light?"
"or you see my face?" aliongea mwajeshi yule wa ki liberia huku akimtazama mtazania alie mbele yake
"hapana hujaona chochote ila kifo! naam kifo kipo mbele yako kina subiri sekunde ifike kichukue nafasi yake" aliendelea kuongea kwa lugha ya kingereza ,alinyamaza kidogo kisha akaendelea....
"watu wana lia watoto wanakufa jeshi la nchi ya liberia linapoteza wanajeshi wake kila kukicha kwa kupambana na waasi ambao wanapata  msaada kutoka kwako na wenzako wengine. kwa tamaa ya pesa mnawa uzia silaha" maneno haya yalimshtua  mtanzania huyu aliekua kafungwa kwenye kiti kwani hakuelewa maada alie iongelea mwanajeshi wa ki liberia
"unajua silaha mnazo wa uzia waasi zimeua wanajeshi wangapi? zime ua watoto wa ngapi? na nifamilia  ngapi zime sambalatishwa kwa vita vina vyo endeshwa na waasi wanao tumia siraha mnazo wauziampaka sasa una shilingi ngapi kwenye akaunti ambayo umeeipata kwa kuuza siraha na . na angekuwa mtoto wako amekufa kwa kuuliwa waasi kwa siraha ulizo uza mwenyewe hiyo pesa inge rudisha uhai wa mwanao?" aliuliza mfululizo kwa sauti huku akaikunja kunja tshirt ya mateka yule na kumtikisa kwa nguvu na hali hii ilimuogopesha mtanzania..
"unacho cha kulipa kwa matatizo mnayo tuletea ?" mliberia aliuliza tena huku akimkazia macho . mtanzania alitikisa kichwa kukataa
"nani jina lako" mwanajeshi aliuliza . na muda wote aliongea kwa lugha ya kingereza kwani ndo ilikuwa lugha pekee ya kuongea na mateka wao ambae hawa kujua taifa lake
"unaitwa nani"
"hassani  " alijibu kwa sauti iliyo kwaruza. hapo wale wanajeshi wengine waliangaliana kwa wao wali mpiga sana hakusema jina wala taifa lake .
"vizuri kijana. naitwa mustaph" aliongea kwa kushusha pumzi na kijitambulisha kwani aliamini mateka wake anaenda kujibu maswali yake japo alihisi kuongopewa jina.
"hivi unahisi tukikutesa ukafa kisha mwili wako ukafukiwa kwenye aridhi ya liberia unafikiri nani ata peleka taarifa hizi kwenu unazani ndugu zako watajua umepotelea wapi?" mwanajeshi mustaph aliuliza na mtanzania aliejitambulisha kwajina la hassani alitingisha kichwa kumaanisha wasinge pata taarifa .
"sisi hatukuhitaji sana wewe hivyo tuna muhitaji mtu alioko nyuma yako . nani alie kutuma unatokea nchi gani?" mustaph aliuliza kwa utulivu . hakuna jibu lolote alilopata kutoka kwa hassani.

kimya!

kimya kikapita..
"where you come from " ali uliza tena kwa utulivu swali hili lilikuwa gumu kwa huyu mtanzania kwani alijua madhara  ya kutaja nchi yake na lazima nchi yake ingemkataa ..(swala ni kwamba aliingia  hata yeye mwenyewe amejikuta kaisha ingia kwenye janga hili bila kutaraji baada ya ku wrong order)
"kijana jiepushe na matatizo ..nakuuliza unatokea wapi"
mustapha aliuliza kwa sauti ya juu
"bwana hili swala halihusiani na nchi yangu na wala mimi sio muuza siraha nyie...." hassan aliamua kuropoka lakini kabla haja malizia sentesi yake kwa wepesi mustaph alisisima na kumshindilia teke la kifua na kumtupa nyuma hatua tatu akawa chini na kiti chake alicho fungiwa..
muda huo huo mustaph akamfuata palepale chini na kuchutama pale alipo anguka chali.
"sasa utasema"  mustaph aliongea huku aki peleka mkono wake kwenye bega la hassan palipokua na jeraha na kuingiza kidole dumba chake kwenye jiraha la risasi begani mwa hassani..
yowe kubwa lili mtoka hassani kwa maumivu makali aliyo yapata nusu aongee kiswahili lakini aliji control na kuugulia maumivu yale kwa kupiga mayowe hakuhitaji wajue taifa lake hata kidogo..
"nani boss wako na unatokea wapi?"

hukujibu

"hassan hua hatuna muda wa kupoteza ... sekunde chache zijazo utakuwa maiti katika aridhi hii ya liberia..
"bora nife kwani mimi sihusiki na biashara za siraha na siwezi kuihusisha nchi yangu kwenye tuhuma hii. mnani lazimisha ni kubali na wakati hamkunikamata na ushahidi wa kuwa mimi nilikuwa nauza siraha" hassani alijieleza..
"wewe ni jeuri.. kwahiyo bora ufe  enhee?" mustaph alisema huku akiingiza mkono mfukoni
"ndio ni bora mniue" mtanzania hassan alisisitiza akiamini kuwa wasinge weza kumuua
"vizuri hasani" mustaph alisema na muda huo alitoa mfuko maarumu na raba bendi kisha  akamvika kichwani ule mfuko mweupe wa prastiki kisha akuchukua raba bendi na kuufanga ule mfuko maeneo ya shingoni ili isipite hewa ,alifunga kwa ustandi na kwakuzungusha shingoni, kichwa  cha hassani kilikuwa ndini ya mfuko wa plastic ambao haupitishi hata chembe ya hewa...
"leo unakufa kifo unacho stahili" mustaph aliongea na kuamulu wana jeshi waondeke wote mule ndani ili mateka afe kifo alicho stahili.

mtanzania huyu hakuamini kilichokua kinatokea pumzi ilikuwa inakata na kwa shangao mkubwa macho yake yakiwa ndani ya mfuko ule alimuona mustaph na wanajeshi wengine wakiondoka mle ndani na kutoka nje . kisha mstaph aligeuka na kumpungia mkono wa kejeli  na kuufunga ule mlango wa mahabusu ndogo ..mustaph hakugeuka tena aliondoka..

Alitamani amuite  amueleze ukweli lakini ikawa ngumu kwake.

Pumzi ilikita macho yake yakavamiwa na kiza akajaribu kuzuia hali ile lakini ikawa kazi bure  picha ya msichana nzuri wa tanzania ikipita kichwani mwake  'mpenzi wangu nakufa'  nafsi yake ilikiri na hapo hakuona tena kila kitu kwenye mwili wake kikazima.

HII NI RIWAYA YANGU AMBAYO ITAWAFIKIA HAPA 2017 MWANZONI NA HUENDA IKATOKA KITABU.  SHARE KWA AJIRI YA MAANDALIZI MEMA YA RIWAYA HII.

0746206428

Wednesday, November 23, 2016

KISASI

SASA INAPATIKANA WHATSUP KWA GHARAMA YA 1500/= KWA MWEZI.
NDANI YA GROUP UTAPATA SIMULIZI KALI YA SEVEN DAYS OF KARALINA PAMOJA NA IBLAME MY BODY .

0746206428 Whatsapp
tupigie uonganishwe fasta.

Monday, November 14, 2016

SIMULIZI: DHIKI

MTUNZI   :iddi siraji

Naitwa iddi siraji, miaka kumi iliopita nilijikuta nikikosa tumaini la maisha na nikipoteza furaha kama waliyo kuwa nayo binadamu wenzangu nilitamani mtu yoyote atokee anishike mkono lakini hakuwahi kutokea na matatizo yakazidi kuniandama matatizo tabu na shida vikawa ni sehemu kubwa ya maisha yangu hii ilinifanya niamini kuwa mungu ananichukia anauchukia uwepo wangu kwenye dunia hii. ndio msaada wa mungu ulikuwa mbali na familia yetu,,,,,unaweza sema nakufuru lakini labda nikikusimulia simulizi ya maisha yangu utaona nipo sahihi katika haya nisemayo,,,,
2006 TABORA
Nilishtushwa kutoka usingizini na matone ya maji ambayo yalini dondokea karibu mwili wangu wote haraka niliamka nikagundua kuwa kulikuwa na mvua kubwa iliyo kuwa ikiendelea kunyesha niliamka haraka nakuanza kupapasa huku na kule nikiwa katika ya giza na katika kupapasa nilifanikiwa kupata toch yangu , nikaanza kuiangakia juu ya kuiwasha maana ilikuwa mbovu mbovu , nilifanikiwa kuiwasha ikatoa mwanga mkali na mara hapo hapo mwanga ukaanza kufifia..
niliangaza na kusogea kwenye kona moja ya.
Chumba nilichokuwemo kona hii
kipande kidogo juu ya paa
nilikuwa nimeenze matawi ya
mahama hivyo palikuwa hapa
vuji nilijisogeza kwenye kona
hiyo na kukaa na kujikunja kwa
ukiwa mkubwa sana na mawazo
mengi juu ya maisha yetu
magumu,. niliinua macho na
kutazama za kuta za chumba kile
zilikuwa ni kuta za miti na
udongo ,na kulikuwa na matobo
yenye uwazi katika kuta hizo
ilikuwa ni nyumba yenye chumba
kimoja na ilikuwa ya zamani ila
ilikuwa imara sana tatatizo la
chumba kile ilikuwa inavuja
sana wakati wa mvua....
Mara ghafla mawazo yangu
yalikatishwa na sauti ya
kugongwa kwa mlango wa
chumba kile kutokea nje ..haraka
niliinuka bila kuuliza ni nani alie
kuwa akigonga nikatoa mti
uliokuwa umeegemea kwenye
mlango na ndo mti huu ulikuwa
umezuia mlango usifunguke ,.
Baada ya kutoa mti huu niliinua
mlango na kuweka pembeni,
hapo hapo nilishtuka kidogo na
nikapatwa na fedheha baada ya
kumuona mama yangu akiwa
kalowa kiasi
"he! mama" niliongea huku
nikimshika mkono aingie
ndani,,,,,"mhh mwanangu nimeamua kuja
humu mwako mvua ni kubwa na
na ule ufa wa nyumba yangu
nimeona kama umeongezeke
tusije tukadondokewa na ukuta
" mama aliongea
mfulululizo na maneno yake
yakanitia simanzi moyoni "ah
hawa mafundi walitutapeli sijui
ndo walijengaje hiyo nyumba"
niliongea huku nikalaani mafundi
walio tujengea"tuna muachia
mungu mwanangu" mama
aliongea kwa unyonge huku
akijisogeza sehemu ambayo
ilikuwa haivuji, nili muonea sana
huruma mama akiwa na mdogo
wangu mgongoni na muda huo
mama alikaa kitako chini pakavu
na kumshusha mdogo wangu
kutoka mgongoni (mdogo huyo
alikuwa anaitwa mussa na
alikuwa ana miaka mitatu
kasoro )
Muda huo niliegesha tena ule
mlango wa chumba kile kisha
nikaanza kutafuta sehemu nzuri ya
kuweka toch ili iangaze mule
ndani na muda huo upepo mkali
ulianza kuvuma na upepo huu
ulipenya ndani kupitia matundu
yenye uwazi mkubwa yaliyokuwa
kwenye kuta za chumba kile,,
"mwanangu mdogo wako
amekamatwa na ugonjwa wake
wa pumu" nilimsikia mama
akiongea kwa sauti nami haraka
nilipiga hatua kadhaa na kusogea alipo kuwa mama na kumuona mdogo wangu aki hangaika kuitafuta pumzi, hii ilisababishwa na upepo mkali uliovuma"hii mitihani ya mungu ,, dawa yake nimeiacha mule ndani mwangu,,, mshike mdogo wako niendee" mama aliongea akitaka anipe mtoto"hapana mama acha niendee mimi""haya mwanangu ipo kwenye tandiko karibu na nipo chagamiaga,,,," kabla mama haja malizia kuongea kilisikika kishindo kikubwa nje ya chumba tulichokuwemo, mimi nikaruka pembeni kwa uoga mkubwa na kukaa chini . kishindo kilikuwa kikubwa mno,,,
"ni nini hicho" mama aliuliza kwa hamaki
mi nilibaki kimya lakini muda huo huo nikakumbuka kuwa nilitakiwa nikalete dawa ya mdogo wangu ya pumu , haraka niliinuka na kujisogeza mlangoni nikachungulia kwenye moja ya tundu ukutani nilikutana na kiza kizito na kupata tabu kutazama lakini muda huo huo radi ilimulika na kuleta mwanga mkubwa nilitazama palipokuwa na nyumba yetu lakini ajabu ni kwamba sikuiona nyumba yetu niliona tu kitu kama kichuguu kidogo!!
Lahaula! Nyumba yetu ilikuwa imeanguka Kumbe kile kishindo tulicho kisikia ni nyumba yetu ilikuwa imeanguka
"mama nyumba yetu imeanguka mama" nilijikuta nikiongea
Lakini mama hakujibu chochote kamya!
Haraka nikageuka alipo kuwa mama na hapo nilimuona mama akiwa busy na mdogo wangu ambae alikuwa anatapatapa kwa pumu....na dawa yenyewe ndio ilikuwa kwenye ile nyumba iliyo anguka ..
Nilimsogelea mama alipokuwa na nilimuona mama machozi yakimtoka akihangaika na mdogo wangu . Hapo hapo wazo lilinijia la kumsaidia mdogo wangu
"mama niende kwa mama pendo atakuwa na dawa nikamfunguze" niliongea huku nikiinuka
"sawa mwanangu fanya haraka tumsaidie mdogo wako" mama alijibu na muda huo nilikuwa nikitoka nje bila kujali mvua giza na upepo mkali , nikuanza kukimbia kuelekea kwa mama pendo,...
Mama pendo alikuwa ni mama aliekuwa akiishi kijiji kile kile tulicho ishi na alikuwa ni nesi wa zahanati yakijiji jirani na alikuwa akifahamiana na mama hivyo safari yangu ilikuwa ni kwenda kuomba msaada kwa huyo mama nakulikuwa na umbali wa mrefu kidog...
Kijiji kilikuwa kimya mvua kubwa ikiendelea kunyesha nikiwa peke yangu katika mvua ile na giza kubwa la kutisha huku nikibahatisha bahatisha njia na mara moja moja radi ilimulika na kufanya kutokee mwanga na kisha giza kutawala tena, mpenzi msomaji sito sahau usiku huo kwani ilikuwa ni giza la kuogepesha lakini sikuwa na woga nilikuwa najaribu kuokoa maisha ya mdogo wangu...,
Niliku nakimbia mchakamchaka nikijaribu kuwahi kwa mama pendo ., nikiwa katika kukimbia nilianza kusikia sauti za maji na hapo nikatambua kuwa nilikuwa nimekaribia kwenye kijito ambacho ukikavuka ndio unafika kwa ma pendo , niliongeza mwendo wa mchaka mchaka .
Nilipo fika sehemu ya kuvuka siku amini macho yangu!
Mbele yangu kulikuwa na mto mkubwa na sauti za maji zilitawala sikuamini kuwa mvua hii imeweza sabisha mto ufurike...
Nilisimama kwamuda lakini nilipo kumbuka hali ya mdogo wangu niliamua kuchuku mti mrefu nakujaribu kuuvuka mto huu huku nikichoma choma mti nijue wapi parefu na wapi pafupi, nilisogea taratibu huku ule mto ukiendelea kupitisha maji kwa kakasi nilijitahidi na kupiga hatua ka tisa lakini maji yale yalikuwa na nguvu na nilipo jaribu kuendelea nilijikuta nikipoteza stamina baada ya mguu wangu wa kushoto kukanyaga kwenye kijishimo, maji yalini zidi nguvu nikajikuta nikielea na kusombwa na maji ! nilijaribu kupiga kelele lakini maji yali ingia mdomoni nikashindwa, maji yalinipeleka kwa nguvu huku nikitapa tapa kujiokoa, ghafla kitu kigumu mithiri ya jiwe kilinigonga kwa nguvu kwenye paji la uso nikapata maumivu na muda huo nikahisi giza zito picha ya mama ikipita kichwani kwangu na giza zito likakubika taswila yangu ....itaendelea..
0746206428

SIMULIZI: DHIKI

MTUNZI   :iddi siraji

Naitwa iddi siraji, miaka kumi iliopita nilijikuta nikikosa tumaini la maisha na nikipoteza furaha kama waliyo kuwa nayo binadamu wenzangu nilitamani mtu yoyote atokee anishike mkono lakini hakuwahi kutokea na matatizo yakazidi kuniandama matatizo tabu na shida vikawa ni sehemu kubwa ya maisha yangu hii ilinifanya niamini kuwa mungu ananichukia anauchukia uwepo wangu kwenye dunia hii. ndio msaada wa mungu ulikuwa mbali na familia yetu,,,,,unaweza sema nakufuru lakini labda nikikusimulia simulizi ya maisha yangu utaona nipo sahihi katika haya nisemayo,,,,
2006 TABORA
Nilishtushwa kutoka usingizini na matone ya maji ambayo yalini dondokea karibu mwili wangu wote haraka niliamka nikagundua kuwa kulikuwa na mvua kubwa iliyo kuwa ikiendelea kunyesha niliamka haraka nakuanza kupapasa huku na kule nikiwa katika ya giza na katika kupapasa nilifanikiwa kupata toch yangu , nikaanza kuiangakia juu ya kuiwasha maana ilikuwa mbovu mbovu , nilifanikiwa kuiwasha ikatoa mwanga mkali na mara hapo hapo mwanga ukaanza kufifia..
niliangaza na kusogea kwenye kona moja ya.
Chumba nilichokuwemo kona hii
kipande kidogo juu ya paa
nilikuwa nimeenze matawi ya
mahama hivyo palikuwa hapa
vuji nilijisogeza kwenye kona
hiyo na kukaa na kujikunja kwa
ukiwa mkubwa sana na mawazo
mengi juu ya maisha yetu
magumu,. niliinua macho na
kutazama za kuta za chumba kile
zilikuwa ni kuta za miti na
udongo ,na kulikuwa na matobo
yenye uwazi katika kuta hizo
ilikuwa ni nyumba yenye chumba
kimoja na ilikuwa ya zamani ila
ilikuwa imara sana tatatizo la
chumba kile ilikuwa inavuja
sana wakati wa mvua....
Mara ghafla mawazo yangu
yalikatishwa na sauti ya
kugongwa kwa mlango wa
chumba kile kutokea nje ..haraka
niliinuka bila kuuliza ni nani alie
kuwa akigonga nikatoa mti
uliokuwa umeegemea kwenye
mlango na ndo mti huu ulikuwa
umezuia mlango usifunguke ,.
Baada ya kutoa mti huu niliinua
mlango na kuweka pembeni,
hapo hapo nilishtuka kidogo na
nikapatwa na fedheha baada ya
kumuona mama yangu akiwa
kalowa kiasi
"he! mama" niliongea huku
nikimshika mkono aingie
ndani,,,,,"mhh mwanangu nimeamua kuja
humu mwako mvua ni kubwa na
na ule ufa wa nyumba yangu
nimeona kama umeongezeke
tusije tukadondokewa na ukuta
" mama aliongea
mfulululizo na maneno yake
yakanitia simanzi moyoni "ah
hawa mafundi walitutapeli sijui
ndo walijengaje hiyo nyumba"
niliongea huku nikalaani mafundi
walio tujengea"tuna muachia
mungu mwanangu" mama
aliongea kwa unyonge huku
akijisogeza sehemu ambayo
ilikuwa haivuji, nili muonea sana
huruma mama akiwa na mdogo
wangu mgongoni na muda huo
mama alikaa kitako chini pakavu
na kumshusha mdogo wangu
kutoka mgongoni (mdogo huyo
alikuwa anaitwa mussa na
alikuwa ana miaka mitatu
kasoro )
Muda huo niliegesha tena ule
mlango wa chumba kile kisha
nikaanza kutafuta sehemu nzuri ya
kuweka toch ili iangaze mule
ndani na muda huo upepo mkali
ulianza kuvuma na upepo huu
ulipenya ndani kupitia matundu
yenye uwazi mkubwa yaliyokuwa
kwenye kuta za chumba kile,,
"mwanangu mdogo wako
amekamatwa na ugonjwa wake
wa pumu" nilimsikia mama
akiongea kwa sauti nami haraka
nilipiga hatua kadhaa na kusogea alipo kuwa mama na kumuona mdogo wangu aki hangaika kuitafuta pumzi, hii ilisababishwa na upepo mkali uliovuma"hii mitihani ya mungu ,, dawa yake nimeiacha mule ndani mwangu,,, mshike mdogo wako niendee" mama aliongea akitaka anipe mtoto"hapana mama acha niendee mimi""haya mwanangu ipo kwenye tandiko karibu na nipo chagamiaga,,,," kabla mama haja malizia kuongea kilisikika kishindo kikubwa nje ya chumba tulichokuwemo, mimi nikaruka pembeni kwa uoga mkubwa na kukaa chini . kishindo kilikuwa kikubwa mno,,,
"ni nini hicho" mama aliuliza kwa hamaki
mi nilibaki kimya lakini muda huo huo nikakumbuka kuwa nilitakiwa nikalete dawa ya mdogo wangu ya pumu , haraka niliinuka na kujisogeza mlangoni nikachungulia kwenye moja ya tundu ukutani nilikutana na kiza kizito na kupata tabu kutazama lakini muda huo huo radi ilimulika na kuleta mwanga mkubwa nilitazama palipokuwa na nyumba yetu lakini ajabu ni kwamba sikuiona nyumba yetu niliona tu kitu kama kichuguu kidogo!!
Lahaula! Nyumba yetu ilikuwa imeanguka Kumbe kile kishindo tulicho kisikia ni nyumba yetu ilikuwa imeanguka
"mama nyumba yetu imeanguka mama" nilijikuta nikiongea
Lakini mama hakujibu chochote kamya!
Haraka nikageuka alipo kuwa mama na hapo nilimuona mama akiwa busy na mdogo wangu ambae alikuwa anatapatapa kwa pumu....na dawa yenyewe ndio ilikuwa kwenye ile nyumba iliyo anguka ..
Nilimsogelea mama alipokuwa na nilimuona mama machozi yakimtoka akihangaika na mdogo wangu . Hapo hapo wazo lilinijia la kumsaidia mdogo wangu
"mama niende kwa mama pendo atakuwa na dawa nikamfunguze" niliongea huku nikiinuka
"sawa mwanangu fanya haraka tumsaidie mdogo wako" mama alijibu na muda huo nilikuwa nikitoka nje bila kujali mvua giza na upepo mkali , nikuanza kukimbia kuelekea kwa mama pendo,...
Mama pendo alikuwa ni mama aliekuwa akiishi kijiji kile kile tulicho ishi na alikuwa ni nesi wa zahanati yakijiji jirani na alikuwa akifahamiana na mama hivyo safari yangu ilikuwa ni kwenda kuomba msaada kwa huyo mama nakulikuwa na umbali wa mrefu kidog...
Kijiji kilikuwa kimya mvua kubwa ikiendelea kunyesha nikiwa peke yangu katika mvua ile na giza kubwa la kutisha huku nikibahatisha bahatisha njia na mara moja moja radi ilimulika na kufanya kutokee mwanga na kisha giza kutawala tena, mpenzi msomaji sito sahau usiku huo kwani ilikuwa ni giza la kuogepesha lakini sikuwa na woga nilikuwa najaribu kuokoa maisha ya mdogo wangu...,
Niliku nakimbia mchakamchaka nikijaribu kuwahi kwa mama pendo ., nikiwa katika kukimbia nilianza kusikia sauti za maji na hapo nikatambua kuwa nilikuwa nimekaribia kwenye kijito ambacho ukikavuka ndio unafika kwa ma pendo , niliongeza mwendo wa mchaka mchaka .
Nilipo fika sehemu ya kuvuka siku amini macho yangu!
Mbele yangu kulikuwa na mto mkubwa na sauti za maji zilitawala sikuamini kuwa mvua hii imeweza sabisha mto ufurike...
Nilisimama kwamuda lakini nilipo kumbuka hali ya mdogo wangu niliamua kuchuku mti mrefu nakujaribu kuuvuka mto huu huku nikichoma choma mti nijue wapi parefu na wapi pafupi, nilisogea taratibu huku ule mto ukiendelea kupitisha maji kwa kakasi nilijitahidi na kupiga hatua ka tisa lakini maji yale yalikuwa na nguvu na nilipo jaribu kuendelea nilijikuta nikipoteza stamina baada ya mguu wangu wa kushoto kukanyaga kwenye kijishimo, maji yalini zidi nguvu nikajikuta nikielea na kusombwa na maji ! nilijaribu kupiga kelele lakini maji yali ingia mdomoni nikashindwa, maji yalinipeleka kwa nguvu huku nikitapa tapa kujiokoa, ghafla kitu kigumu mithiri ya jiwe kilinigonga kwa nguvu kwenye paji la uso nikapata maumivu na muda huo nikahisi giza zito picha ya mama ikipita kichwani kwangu na giza zito likakubika taswila yangu ....itaendelea..
0746206428

NGULI ABUNUWASI

HEKAYA ZA ABUNUWASI
HEKAYA ZA ABUNUWASI ni kitabu cha hadithi za kusisimua, zinazofurahisha sana kutokana na umahili wa watunzi wa vitabu vya kale. Kutokana na utamu wa hadithi za ABUNUWASI, Blog ya MPIGANAJI itawaletea hadithi hizo ili kuwachangamsha akili...............
KISA CHA ABUNUWASI NA MFALME
SIKU moja alfajiri, wakati wananchi wa mji wenye wakazi wengi walipokwenda kuchota maji mtoni, walishangazwa kuuona mkono wa mtu ukiwa katikati ya mto. Mkono huo wa ajabu ulikuwa umenyoosha vidole viwili juu, kuonyesha alama ya mbili.
Wananchi walistushwa sana na kitendo hicho, wakaogopa hata kuchota maji mtoni, kwani hawakuwahi kuona tukio la kuogopesha kama lile. Wengine waliamini kuwa huo ulikuwa mwili wa mtu aliyetupwa mtoni.
Lakini ishara iliyoonyeshwa na mkono huo iliwafanya wananchi waamini kuwa huo ulikuwa mkono wa ajabu. Katika kiza kinene kilichozunguka ndani ya vichwa vya wananchi, habari zikamfikia Mfalme wao, naye akafika haraka eneo la tukio.
Mfalme wa nchi hiyo baada ya kujiridhisha kuwa ulikuwa mkono wa ajabu na uliwekwa na watu wenye imani za kishirikiana, alitoa siku tatu mkono huo uwe umeondolewe, vinginevyo ataleta wataalam kutoka sehemu mbali mbali duniani kwa ajili ya kubaini wahusika.
Siku tatu zilizowekwa na Mfalme zikaisha, wataalam wa mambo ya asili kutoka sehemu mbali mbali duniani wakaanza kuwasili mtoni hapo kwa lengo la kuundoa mkono huo wakashindwa.
Mfalme akatoa ofa nono, waganga wenye sifa na jeuri ya mambo ya jadi wakamiminika eneo la mto, wakafanya mitambiko na mambo yao kwa ufanisi zaidi, wengine wakalala mtoni kuonyesha umahili wao lakini wakashindwa na kuuondoa mkono huo wa ajabu...
Mfalme na wasaidizi wake wakakuna vichwa, wananchi hawana jinsi ya kupata maji. Maji mtoni hayachoteki, wananchi wanaogopa kutumia maji hayo. Ndipo Abunuwasi akajitokeza mbele ya Mfalme. Akamwambia Mfamle, "Mimi naweza kujaribu.
Mfalme akamfukuza Abunuwasi kwa hasira, akamwambia. "Mpumbavu sana wewe, hapa wameshindwa waganga na waganguzi, wewe Abunuwasi utaweza wapi, usitupotezee muda wetu".
Abunuwasi akaondoka, waganga wakazidi kumiminika mtoni wakitoka sehemu mbali mbali za dunia kutokana na sifa zao. Kila walichofanya kuuondoa mkono huo wakachemka na kuondoka eneo hilo kimya kimya.
Abunuwasi akamrudi Mfalme, akamwambia,  "Wacha nijaribu mimi". Mfalme akamjia juu akamwambia. "Nimesema huwezi Abunuwasi, wameshindwa waganga wa dunia, utaweza wapi wewe?, Abunuwasi akasisitiza. "Wacha nijaribu mimi kama walivyojaribu wengine na kushindwa.
Mfalme kwa hasira akamwambia Abunuwasi, "Haya jaribu, maana unataka kutupotezea muda tu hapa, lakini ole wako ukishindwa, nitawaamru askari wakutie ndani".
Abunuwasi akaanza kuuzunguka mto huku umati wa wananchi ukimwangalia kwa makini, alipita huku na huku akikimbia kama mtu aliyepatwa na wazimu, Mfalme akaanza kuchukia, hatmaye Abunuwasi akakaa sambamba na mkono ule, Abunuwasi akachuchumaa chini na kuinua mkono wake juu mfano wa mkono ule.
Mfalme na wananchi walikuwa kimya wakifuatilia kwa makini tukio hilo, Abunuwasi aliuchezesha mkono wake kushoto na kulia, mkono ule ndani ya maji nao ukafanya vile, kama alivyofanya Abunuwasi. Wananchi wakashangazwa mno na kitendo kile.
Abunuwasi akauvuta mkono wake nyuma, mkono huo pia ukafanya hivyo, Abunuwasi akakunja kidole chake kimoja, mkono ndani ya maji nao ukafanya vile. Hatmaye Abunuwasi akaushusha mkono wake chini kama anaudhamisha, mkono ule nao ukadhama na haukuonekana tena.
Mayowe, vigelegele na shangwa vikasikika, Mfalme akasimama akamfuata Abunuwasi, akamuomba radhi, akamtukuza na kuonyesha kufurahishwa. "Ahsante sana Abunuwasi, umetuondolea aibu, nisamehe kwa kukudharau, sikutegemea kabisa".
Wananchi wakaja juu wanamtaka Abunuwasi apewe Ufalme. Maana ameweza kufanya jambo lililowashinda waganga na waganguzi. Mfalme akahamaki. Abunuwasi akaula...

Saturday, November 12, 2016

PACHA WANAO FANANA :1

RIWAYA:Pacha Wanaofanana

MTUNZI:Agness Matimba

SIMU:0757 143665/0714 215231

SEHEMU YA KWANZA.

ILIKUWA ni majira ya saa tatu za usiku. Mvua ya rasharasha ilikuwa imetanda katika kijiji cha Mtakuja,huku katika nyumba moja iliyokuwa kuu kuu ambayo haijulikani kwa mara ya mwisho ilifanyiwa ukarabati lini.Iilisikika sauti ya Bibi mmoja aliyejulikana kwa jina la Bi.Nyamtaka.Ilikuwa ikisisitiza kwa sauti,
"Catherine jitahidi sukuma,sukuma kwa nguvu.Mbona huyu mmoja ameshatoka".Sauti ya Catherine ikasikika,
"Siwezi Bibi nimechoka jamani",
"Jikaze mjukuu wangu, upo tayari kumpoteza mwanao?".Bi.Nyamtaka aliuliza,lakini ghafla chupa ya uzazi ilimalizika kupasuka.
Bi.Nyamtaka alimlaki mtoto kwa mikono miwili huku akimpokea kwa kusema.
"Ni wa kike tena. Wote ni wa kike".Catherine akatamka kwa sauti yenye uchovu,
"Kulwa ataitwa Maria na Doto ataitwa Mariam".
Bi.Nyamtaka alimfunga Kulwa kwa kutumia khanga ya bluu halafu Doto alimfunga khanga ya bluu bahari.Catherine alifurahi sana baada ya watoto kupatiwa huduma muhimu.
Catherine alipatiwa wanae aliwanyonyesha huku akiwaangalia kwa kutumia mwanga hafifu wa koroboi kuu kuu ambayo nayo kama ile nyumba, haijulikani kwa mara ya mwisho ilifanyiwa usafi lini.Baada ya kuwanyonyesha watoto wake hatimaye Catherine alilala usingizi mzito huku watoto wakiangaliwa na Bi.Nyamtaka.
***********
Siku iliyofuatia Bi.Nyamtaka akawa anawaangalia watoto wanatofauti gani katika miili yao maana walifanana sana.Na alimwambia Catherine kuwa kama watoto wale hawatagundulika na tofauti ni lazima moja atamtoboa katika sehemu ya mwili wake.
Hakika walikuwa ni watoto wazuri. Walifanana kila kitu.Kwa bahati nzuri Bi. Nyamtaka akagundua tofauti moja Kulwa alikuwa na alama ya kidoti kidogo sana karibu na pua, lakini Doto hakuwa nayo hivyo alimueleza Catherine na kumuonyesha asije akawachanganya.
***********
Catherine aliwapenda sana watoto wake, huku Bi.Nyamtaka akijitahidi kumsaidia kwa ukaribu kabisa kuwalea watoto wake kwa kuwapa malezi bora.
Catherine alikuwa mtu wa kukaa nyumbani.Bi.Nyamtaka akawa anapika pombe za kienyeji kwaajili ya kuwapatia kipato ambacho Kitamsaidia yeye na Catherine kwa kupata chakula na mavazi.Hata hivyo Catherine alijisikia vibaya sana akaona anampa mzigo Bibi yake.Hivyo moyoni alipanga yake,hakutaka kukaa sana kwa Bibi yake.
Baada ya miezi mitatu watoto wake walikuwa wamekuwa wakubwa kidogo wakiwa na afya tele.Catherine alianza kuwanywesha uji maana walishaanza kumchosha kwa sababu walikuwa wananyonya sana.
Siku moja jioni Catherine akiwa amekaa na Bibi yake nyumbani ndipo alipoamua kutoa dukuduku lake la moyoni kwa kumwambia Bibi yake anamaongezi naye muhimu.Bi.Nyamtaka bila ya hiyana akamwambia Catherine,
"Nakusikiliza mjukuu wangu niambie"Catherine alisawazisha koo lake vizuri kwa kukohoa kidogo.Huku akimwangalia Bibi yake,akaanza
"Ahsante sana Bibi kwa kunipokea na kunitunza tangu nilipokuja hapa kijijini nikiwa na mimba ya miezi miwili.Sasa hivi najiona kama nimekuletea mzigo mkubwa wa vitukuu wawili na mimi nahitaji kula pamoja na mavazi".Akatulia kidogo na kumuangalia Bibi yake aone atasemaje. Alipoona kimya,akaendelea,
"Nimeona nakuletea mzigo mkubwa sana hivyo nakuomba niruhusu niende mjini nikatafute maisha kwaajili ya wanangu, ikiwezekana na wewe pia niwe nakutumia hela kidogo kwaajili ya matumizi".Bi Nyamtaka alishtuka,akasimama huku akijifunga vizuri kanga yake kuu kuu iliyokuwa imetoboka.Akamwambia Catherine,
"Mjukuu wangu sikuruhusu kuondoka. Unatakiwa ukae nyumbani uwalee watoto wako.Isitoshe una watoto mapacha utaweza kuhimili mikikimikiki ya safari pamoja na kuwabeba watoto?"
"Ndio nitaweza Bibi naenda kutafuta maisha Bibi kwaajili ya wanangu na wewe Bibi. Wewe ndiye mlezi wangu uliyebaki kwaajili yangu, Bibi tafadhali niruhusu"Catherine alikuwa amemjibu Bibi yake hivyo.
Bi. Nyamtaka alikataa katukatu, hakumruhusu Catherine kurudi mjini tena.Catherine alikosa raha, alikaa kwa Bibi yake kwa shingo upande akiwaza afanye nini ili Bibi yake amkubalie kuondoka.
Baada ya siku tatu Catherine akiwa amejipumzisha alipata wazo akubaliana na wazo lake akapanga cha kufanya,wazo lililokuwa kichwani mwake ni kutoroka pale kwa bibi yake.
[SAFARI YA KUTOROKA]
Alfajiri Catherine alishtuka kutoka usingizini, akaamka na kumwamsha Bi.Nyamtaka kwaajili ya kujiandaa kuelekea sokoni.Bi.Nyamtaka akamshukuru Catherine kwa kumwamsha.
Bi.Nyamtaka alipoondoka.Catherine alianza kukusanya nguo za wanae na za kwake akaziweka kwenye rambo vizuri,na kwa bahati nzuri kulikuwa na begi lililokuwa limetoboka kwa kushambuliwa na panya pamoja na mende,hivyo mfuko ule wa rambo akauweka ndani ya begi lile.
Hakutaka kuoga. Alichukua maji akasukutua, akawabeba watoto wake. Mmoja alimbeba mgongoni mwingine akambeba mkononi. Kabla ya kuondoka akaangalia chini ya kitanda, kulikuwa na chungu kidogo ambacho Bi.Nyamtaka alipenda kuhifadhia hela za akiba.
Alikuta akiba wa shilingi elfu ishirini akaichukua na kuandika ujumbe kwa herufi kubwa.
BIBI USINITAFUTE NARUDI KWETU, NIMEYACHOKA MAISHA YA HAPA KIJIJINI.Catherine akaondoka.
Alitembea kwa miguu huku akiwa amevaa khanga zilizotoboka na kandambili tofauti ambazo zinajulikana kwa jina la almaarufu kama la "papa na nguru".Baada ya kutembea kwa muda wa nusu saa huku anga likiwa limetanda na ukungu mweupe wa asubuhi,ndipo alifanikiwa kufika kituo cha mabasi yaendayo mikoani.
Catherine alifanikiwa kupata basi ambalo lilikuwa likitokea pale kijijini kwao na kuelekea jijini Dar-es-salaam.Catherine akaingia kwenye basi na kupishwa siti na kijana wa makamo. Kisha mtoto wake mmoja akasaidiwa na mama mmoja aliyekuwa amekaa siti ya jirani yake. Hapo ndipo akapata afueni kidogo.Akiwa amempakata Maria, Catherine akawa anawaza huku analia.Alijikuta akisema kwa sauti kubwa
"Sitamsamehe".Yule mama aliyemsaidia mtoto akamuuliza,
"Hutamsamehe nani?"Catherine alibaki kimya, akaishika khanga yake iliyokuwa imetoboka akajifuta machozi huku akisema...

JE CATHERINE ALISEMA NINI?

ITAENDELEA KESHOKTWA JUMAMOSI******.

Thursday, November 10, 2016

KAA MKAO WA KULA

Je?ni simulizi ipi ungependa iwe ya kwanza kuchapichwa kitabu kati ya DUNIA INA NICHUKIA na MUHANGA..
toa maoni 0746206428 whatsapp.

Wednesday, November 9, 2016

Abdul

RIWAYA : DUNIA INANICHUKIA
simu      : 0746206428

           4

ILIPOISHIA....
Yule mtu aliekuwa akifuatwa nyuma na askari bila yeye mwenyewe kujua alitembea kwa haraka akisunta ili aivuke barabara alioiona mbele yake, kutokana na waswasi na mawazo pamoja na kelele ya mvua iliyo piga kwenye bati za nyumba za mitaa hiyo, huyo kijana hakusikia kabisa muungurumo wa gari la polisi lilokuwa likija katika barabara aliyokuwa akiiwahi ili avuke,
alipoingia tu barabarani mikono yake ikiwa bado kwenye mifuko wa koti ndipo kwa kihoro kikubwa macho yake yaliishuhudia gari ya polisi ikija kwa kasi alipo simama!
ENDELEA.....
"ni abdul"
dereva wa gari alibabaika kumuona abdul akiwa katikati ya barabara na kabla haja fanya lolote, kwa wepesi ambao haukutalajiwa abdul alijitupa pembeni huku akitoa mkono wake wakulia kwenye koti!
, pah pah !, miliyo ya risasi ili sikika huku abdul akijitupa pembezoni mwa barabara,
<*muda wote abdul alipo kuwa anatembea mkono wa kulia ulikuwa umeshika bastola ndani ya koti na kipindi anajitupa pembeni   alichomoa mkono wake kwenye koti na kufyatua risasi mbili akiwa hewani kuilekea ile gari ya polisi ,
abdul baada ya kujitupa chini akiwa anataka ainuke aangalie sehemu ya kujificha hapo hapo akasikia milipuko mikubwa ya risasi na muda huo akashuhudia baadhi ya risasi zikichimba kuta za nyumba za eneo hilo, abdul akabaki pale chini akiwa hana cha kufanya kwani risasi zilikuja kwa wingi eneo alili kuwepo maji yakiwa yamemfika shingoni.
****
robert akiwa anaendesha gari kwa kasi mara alisikia ile milipuko ya risasi ikitokea upande aliokua akielekea moyo wa robert ukaripuka kwa furaha akijua abdul kaonekana"yah hisia zangu zilikwa sahihi upande wa magharibi ndipo alipo kimbilia abdul" alijisemea robert huku akijisifu kwa uhodari wa kuhisia , mara ghafla akasikia milipuko mingine mfululizo ikitokea upande wake wa kulia, robert alipigwa butwaa kwani alisikia milipuko ya risasi pande mbili tofauti hakutaka kuamini kule aliposikia risasi mara ya kwanza ndiko aliko sikia mara ya pili ilikuwa ni sehemu mbili tofauti , robert akiwa anaendelea kujiuliza hapohapo radio call yake ikatoa mlio wa mkoromo,
"inspector robert naongea" alisema robert baada ya kusogeza radio call kinywani mwake,
" ehh afande tumevamiwa huku na wenzetu wa nne wamesha uliwa ndani ya guest walio enda kukagua" sauti iliongea ya upande wa pili ,"unafikiri atakuwa ni abdul" aliuliza robert,
"nafikiri maana wenzetu waliingia kukagua kwenye guest hiyo na mara wakashambuliwa ndani ya guest, na walio shambulia wapo zaidi ya mmoja kwa kifupi tunaomba msaada msaada" taarifa hii ilimchanganya robert robert alijiuliza ina maana abdul alikuwa na kundi lake huko tandika 'yah inaweza ikawa ndomaana aliamua kukimbilia huku' alijijibu robert,
"hemu muulize guest ina itwaje" sauti ya mwenye kiti iliuliza kutokea nyuma ya robert,
"ah wazo zuri.... eti we hiyo guest inaitwaje" robert aliongea na watu wawili kwa wakati mmoja,
"ah eh ni coconut guest"
"washa gari twende na pajua"alisema mwenye kiti,
"sawa lakini acha ni wape kwanza taarifa askari wote" alijibu robert,
robert akawaalifu askari wote waliokuwa kwenye oparesheni waelekee coconut guest kwani huko ndiko waliko shambuliwa wenzao.
robert alipo maliza akawasha gari na kuanza kuondoka .
<<<*****
askari waliokuwa mtaani baada ya kufanya msako bila kufanikiwa waliamua waanze kusogea upande wa upande wa magharibi kama walivyo ambiwa na robert, gari lenye askari kumi na moja lilianza kuondoka kuelekea magharibi na ni hili gari ambalo askari wake walikutana na yule muogota kopo alie waelekeza alipo muona abdul. na gari la pili lili ondoka na askari kumi na mbili gari hili lilipita barabara nyingene, baada ya mwendo wa kasi dreva wa gari lenye askari kumi na mbili alisimamasha gari baada ya kuona bar moja na guest moja pamoja na grocery moja ndani ya mtaa alio kuepo akaona ni vyema washuke na wakague ile guest na bar pamoja na grocery. "oya shukeni tukague eneo hili fasta tuondoke.... wanne muende kwenye ile guest na wanne wengine waende kukagua kwenye ile bar na watatu mnifuate tukakague ile ile grocery", alisema dreva alie onekana kuwa kiongozi wa askari wale. kulitokea ubishi kidogo kwani kuna askari nane wali gombea kwenda kwenye guest kukagua , hii ilitokana na askari hawa kila walipo enda kukagua guest wali vunja milango ya vyumba ambamo wali kuta baadi ya watu wakiwa wakifanya mapenzi na wali wakuta wakiwa kama walivyo zaliwa kitendo hiki kikapelekea askari kupenda kukagua guest kuliko sehemu nyingine , yule askari alie kuwa anaongoza askari hao ali wakemea baada ya kuona wana leta masihara kwenye kazi,
"haya bwana nendeni mkawachungulie vizuri" alisema askari mmoja katika wale wanane huku akijitoa kwenye kundi lile na wenzake watatu wakafuate,
"bwana sasahivi sio zamu yenu tuachieni tukajionee vibwanga" alisema askari mmoja kati ya wale wanne walio baki.
msako ukaanza na wale askari waliokuwa wamepangwa kukagua guest walitembea haraka na kuingi ndani ya guest hiyo iliyo itwa coconut guest, askari wale wakatoa taarifa juu ya msako wao ndani ya guest na wakaanza kukagua,
walivyo fika kwenye korido ya vyumba vya guest wakajigawa wawili wawili ili waanze kukagua vyumba vile,
askari wawili wakagonga chumba kimoja wakafunguliwa wakaingia waanze kukagua, na askari wawili wengine waka gonga chumba kilichofuata ... kimya! hakuna aliitika wala kufungua chumba kile.
askari hawa wawili askari wawili wakaangaliana wakajua mule ndani kilicho kuwa kinaendelea ni mapenzi , askari hao wakapeana ishara kuwa wavunje mlango ili wakajionee mambo, askari mmoja akarudi nyuma na kuurukia teke mlango ukafunguka na ghafla askari alie bomoa mlango akatupwa kwenye ukuta na kuanguka chini kama mzigo! na mlio wa risasi ukasikika! askari wapili alipigwa butwaa hakujua mwenzake katupwa na nini, askari akainua bunduki yake kuelekea kwenye kile chumba lakini alichewa kwani hapohapo risasi mbili zili toboa kifua chake zikitokea kwenye chumba walicho bomoa mlango! askari wawili wakawa chini huku mmoja akiwa na tundu likivuja damu kwenye paji la uso wake. wale askari wengine walioingia kwenye chumba cha kwanza walisikia ile milipuko ya risasi iliyo tokea chumba cha pili wakatoka haraka ili wawa saidie wenzao lakini walikua na bahati mbaya kwani walivyo tokeza tu kwenye korido walipokelewa na risasi mfululizo zilizo toka kwa watu wawili walio simama kwenye maiti za wenzao. watu hao wawili baada ya kuona askari wanne wamesha kufa, watu hawa wawili wakaingia kwenye chumba walicho kuwemo wakachukua mabegi yao mawili yaliojaa wakaanza kukimbia wakitoka nje ya guest askari .
*** wale askari wanane walio kuwa wanafanya msako kwenye bar na grocery walisikia ile milipuko ya risasi kutokea kwenye guest walio ingia wenzao ndipo wakaanza kukimbia kwenda kuwa saidia wenzao,
"itakua ni abdul kashambulia tuwahi tuka wasaidie wenzetu" alisema yule kiongozi huku akitimka mbio.
walivyokua wanaiingia ndani ya guest ile ndipo wakaona wale vijana wawili wenye mabegi wakiwa na bastola mikononi mwao wakitokea kwenye korido walikua kama umbali wa hatua thelasini askari hawa kusita walianza kuwatupia risasi wale watu ambao nao kwa wepesi walijitupa chini waka biringita kuridi kwenye korido ambapo walipata cover na kuanza kuwatupia risasi askari bila kuwa pata kwani askari nao walikuwa wame jikinga kwenye ukuta wa counter, asakari na wale watu wawili wakaendele kutupiana bila kupatana.
yule kiongozi wa askri wale alivyo iona hari ile ndipo alipo amua kumpa taarifa robert juu ya tatizo hilo la coconut guest.
*****>>>
taarifa alietoa robert ilizagaa kwa askari wote ndani ya oparesheni ile askari wakaanza kumiminika kuelekea coconut guest,
robert nae kwa kuelekezwa na mwenye kiti akafanikiwa kufika coconut guest na magari mengine ya polisi yakafika eneo hilo na askari wakazunguka guest hiyo bundiki zao zikiwa makini mikononi mwao, askari wakaanza kujiandaa wavamie ndani ya guest hiyo........
je? hawa watu wawili walio ua polisi wanne ni kina nani? kwani wame ua polisi?
je?nini kitawakuta maana wamezungukwa na asakari.
upande wa pili abdul alijitupa chini na kuachia risasi mbili, lakini kipindi anataka kuamka ana shuhudia risasi zikitua eneo alipo na risasi nyingine zina chimba kuta za eneo hilo je? abdul atapona hapo?
tukutane kesho saa tisa upate kujua mengi zaidi.

Iblame my body

RIWAYA   : I'BLAME MY BODY ( NAULAUMU MWILI WANGU ) Imezaminiwa na   Simulizimahiri.blogspot.com Mahakama kubwa ya kesi za jina...