Friday, January 6, 2017

PENZI LA FUKARA

RIWAYA PENZI LA FUKARA MATESO

MTUNZI : ZUBERI MARUMA

WHATSUP : 0652281153

CHAPISHO NO 01

(FUMBO LILILOFUMBWA)

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI

Kila ninapojaribu kufumba macho yangu nikusahau uwa nashindwa.

Siuamin moyo wangu kama kweli ipo  siku ungeniacha

Tena katika kipindi ambacho nakuitaji zaidi.kipindi ambacho ndo ningetakiwa nile  matunda ya masomo yako

Leo hii Mimi na wewe tumekuwa kama paka na panya

Lazima nilipize kwa ulilolitenda?!

                   ************

Uso  wake ulikunjamana kwa hasira,mapigo yake ya moyo yaliongezeka kila muda ulipokuwa ukipotea,

Akalifungua kabati lililokuwa Mbele ya macho yake na kupeleka mkono ndani ya kabati lile,akawa anatafuta kitu katikati ya nguo

Akakipata

Ilikuwa ni bastola ndogo,akaiangalia kwa sekunde kadhaa na kuipachika kibindoni

Akalifunga vizuri kabati lile

Hakika moyo wake ulijaa majonzi,simanzi
,sononeko,maumivu tele yaliushambulia moyo wake....

kama kulia alishalia sana mpaka machozi yakamkauka!

maumivu makali yalikishambulia kichwa chake! yamkini ni kutokana na msongo wa mawazo ama kitendo chake ya kulia sana.....

kulilia mapenzi.

Akalifata droo lake akalifungua na kutoka na kalamu na karatasi akakaa katika meza na kuanza kuiandika barua,

huku machozi mepesi yakiloanisha mashavu yake na baadhi ya matone yakiangukia karatasi lile...

barua ile aliianza kwa kuiandika hivi:

"Kwako mpenzi SHONAIZAR!,

najua u mzima wa afya!,mimi kifikra sipo vizuri!
sidhani kama utaniuliza kwa nini!

sababu nadhani waijua

ila tambua kama mapenzi ni hisia!, hisia zangu zilikuwa kwako , uliniteka kifikra sikutaka nichomoke moyoni mwako, ulinifanya mfungwa katikati ya moyo wako, sikuona mwanamke kwa uzuri afikiaye umbo lako...

Ulitumia udhaifu huo kuntesa mwenzako, ni ahadi ngapi ulini ahidi kwamba utonisaliti?!, ni mara ngapi ulinambia kwamba UNANIPENDA sana?!,

kumbe wewe ni mwanahizaya ulojaa unafki eeh!?!...au kisa mimi ni fukara?,au kisa sina pesa?!

shone penzi langu kwa gharama yoyote lazima litalipwa!, machozi yangu niyatoayo kwa sababu yako yatakugarimu my x!,

tambua kama uliunyakua moyo wangu kwa kuni adaa kwamba unanipenda,

malipo yako nitakunyanganya roho yako,...

leo nayachukia mapenzi

kumbuka wewe ndo ulinifanya niyapende!

nakumbuka kipindi kile kwa mara ya kwanza tulipo onana, ndo kwanza ulitoka masomoni TABORA GARLS na kuja kijijini kwetu kufanya utafiti wa mimea na majani ukiwa na wenzako

mimi nikiwa mchungaji wa Mbuzi ndo kazi nlostaili kwa kipindi kile.

mbona marafiki zako wote walikukimbia pale nyoka mwenye sumu kali alipokugonga?

ZUBERI nikajitolea SHONAIZAR kukusaidia!

kosa langu lipo wapi hapo?

najuta kukufahamu

CHOZI LANGU LAZIMA LILIPWE

niliamua kukuchukua mpaka nyumbani kwangu nilipo kuwa naishi peke yangu

nikaanza kuku hudumia kwa madawa asili mpaka ukapona....

Malipo yangu yalikuwa nin?!
kama si kufungwa?

ulishindwa kunsaidia pale marafiki zako walipokuja na wazazi wako wakanikamata heti nimekuteka!!

msaada wangu ukawa adhabu kwangu ,kwa mara ya kwanza mchunga mbuzi kutoka kijijini nikaingia mjini nikiwa chini ya ulinzi mkali!

nyumbani kwangu pakawa segerea!

yani ung'atwe na nyoka nkuchukue nkutibu nionekane nlikuteka?! ila yote nilivumilia,

ulikuja kuniangalia!

na dhamana ukanitolea!, ukisema wazi kwamba mimi ndiye niliyekusaidia! nadiriki kusema msaada wako ndo ulikuwa huo kwangu!

mpz nishkuru kwa ilo!

kwa kunitoa mahabusu na kunitafutia kazi DAR!

sawa pengine labda kwa kuwa sikujua lengo lako mpaka pale ulipontamkia kwamba UNANIPENDA wewe ndo ulinambia siyo mimi niliyekutamkia!.

.kama kweli ulikuwa unanipenda iweje leo hii uje unsaliti?! utamu wa penzi lako ugeuke shubiri kwangu?

naapa my! lazima penzi langu utalilipa!...

hata ikibidi kwa ncha ya upanga!

ila sitokuacha mzima ama zangu ama zako!

SHONE mpenzi kumbuka!!!.....

nilikukubali kwa kuwa u! mwanamke mrembo,mwenye wajihi wa "black beuty" na macho malegevu kama unasinzia!,

dimpozi mashavuni, ulijaliwa miguu minene ya bia!, ni vigumu kwa mwanaume kukataa ombi lako!...

ni mara ngapi ulililia kifuani kwangu?, 

ukinielezea jinsi unavyonyanyasika kwenu?! kisaa.....

hata ulivyonielezea stori yako ya maisha, iliniuma mpenzi sikusita kulia kwamba mama yako alishafariki na sasa unaishi na mama wa kambo, 

anayekunyanyasa kwa masimango bila huruma kukupatia!  sikuweza kuzuia machozi kunitoka!

shetani mkubwa wewe!

nilikulilia nikikuonea huruma kwa nini nisingekuacha ukateseka? nakuchukia wewe mwanamke! nawachukia wanawake wote.....

sababu ikiwa ni wewe kahaba mmoja!

nitaridhika nitakapo ugawanya ubongo wako! kwa furaha sitosita kuula kwa ukatili ulontendea nipo tayari kufungwa,nipo tayari kunyongwa,pindi nikisababisha mauti yako....

KWA NINI KIJANA HUYU ANA HASIRA HIVI KIPI KIPO NYUMA YA PAZIA ITAENDELEA

UKITAKA VIPANDE VYA MBELE VYA RIWAYA HII JIUNGE NA GRP LA MALIPO WHATSUPP 1500 KWA MWEZI PATA VIPANDE 20 KWA 1000

No comments:

Post a Comment

Iblame my body

RIWAYA   : I'BLAME MY BODY ( NAULAUMU MWILI WANGU ) Imezaminiwa na   Simulizimahiri.blogspot.com Mahakama kubwa ya kesi za jina...