Friday, January 6, 2017

RIWAYA YA ROAD TO 2017

RIWAYA : ROAD TO 2017

SEHEMU YA PILI.

31 DECEMBER.

ILIPO ISHIA..
"Hatuna haja ya kuuana sisi kwa sisi leo usiku mtapata damu ya kutosha na gozola atalizika.... kuna watu wanakuja kupitia ukanda huu leo leo wote sita watakuwa chakula chetu usiku huu" bibi yule kizee aliongea kwa sauti ya juu huku kichwani mwake akiwaona wale watalii wakiendeshwa na baraka....!

"ndio wanakuja kupitia barabara jirani leo tutafurahia damu zao" aliongea tena kwa msisitizo.

Endelea..
USIKU WA KAFARA.

Wote walikuwa kimya hata gola nae hakusema kitu.
"haya kila mtu arudi mahali pake na binti wa mama diana ahifadhiwe mpaka nitakapo rudi kutoka ndani" yule Mzee ali waamulu
"sawa malikia" wote walijibu na kuanza kurudi sehemu waliyo kaa mwazo huku mzee juma akimuhifadhi vizuri yule binti kigoli diana.. na yule malikia kikongwe akarudi tena pangoni aakanene na gunzani.

*****************

Baraka aliendesha gari kwa speed tena kwa umakini mkubwa
"Dah hawa askali wametupotezea muda mwingi sana" baraka aliongea na kuvunja ukimya wa punde
"Ah ila mimi niliogopa sana nilipo muona yule askali katoa bunduki kwenye gari yako " sauti ya msicha mmoja kati ya wale watatu aliongea
"Umeonae dolla ...halafu wewe baraka unatabia mbaya kumbe una bunduki humu muda wote huja tuambia" msichana mwingine alidakia kumuunga mkono msicha dolla namsichana huyu alie dakia aliitwa Neema

"AH vitu vidogo sana kumiliki bunduki kama ile kwangu kama fimbo tu" baraka aliji gamba

"ehee ulisha anza kujisifu mr misifa ...sio ajabu hata hajui kuitumia bunduki yenye" sauti ya kiume kati ya wanaume watatu ndani ya gari ile ili msanifu baraka kwa kumtania

"Umeonaeeh john kaishaanza kujisifu" kijana wa tatu aliimuunga mkono john . nahuyu  aliemuunga mkono john aliitwa   Gadyson huku

wote wakicheka...

Kabla kicheko chao hakijaisha baraka alikanyaga brek ya ghafla kisha wote wakayumba kwa kwenda mbele na kurudishwa nyuma na muda huo baraka akashuka na kwenda kuufungua mlango wa nyuma kabisa kulipo kuwa na mizigo akaipekuwa na kuichukua ile bunduki akarudi nayo kwa wenzake akaingiza mkono mfukoni akatoa mfuniko wa simu akamkabidhi john na kumwambia auinue juu mfuniko ule..

"ENHEEE hivyo hivyo uinuie juu nataka ni ulenge niupige risasi huo mfuniko" baraka aliongea huku akirudi nyuma akawa anaikoki kwa kuvuta kitasa kichoopo juu ya bunduki ile
"ahh acha boya wewe" joh alimaka huku gadyson akitaka kuingia chini ya kiti na muda huo baraka akaanza kuwacheka
"mbona mmeogopa si mmesema sijui kuitumia"  baraka aliongea huku maneno yake yakiambatana na kicheko....muda huo wasichana walikuwa wakicheka kwani wanayajua masihara ya hawa vijana watatu..
"haya tazameni jinsi ya kuitumia " aliongea na wote wakamtazama
"ukitaka kupiga una vuta hiki chuma cha standby kisha hii triger unaibonyeza kwa kidole cha shahada ..." aliongea kisha akageuka akailekezea bunduki mstuni  na kufyatua risasi na mlipuko mkubwa ukasikika pale na wale wote watano waliziba masikio
"HAPPY NEW YEAR"  baraka alilalama kwa sauti ya kusherehekea
"Oya mzee wa manchester tuondoke naona ushaanza sifa zako" gadyson aliongea baraka nae akarudisha ile bunduki huku akicheka
"kumbe wa oga .. " aliongea huku akifungua mlango wa nyuma akaiweka juu ya mizigo akafunga mlango akaingia kwenye uskani..

"Yani huyu jamaa kila kitu chake anacho penda kibaya hilo bunduki lake bovu bovu sauti yake mbaya hata mwizi akija na mshale ana kutagisha... bado timu unayo shabikia mbovu....unavyo penda vyote vibovu kasoro demu wako neema"  john aliendeleza tena utani huku wale mabinti wakicheka
"acha wewe huyo movic ana goli kumi na moja bado mbili amkamate coasta then spurs man city asanal tupo nyuma yao tuna wakimbiza na baiskel lao la miti..nyie acheni timu yangu noma "baraka aliongea huku akianza kuchochea speed

"Ila hawa watu wana masihara sana wamenifanye niwe na furaha sana huu umekuwa mwaka mpya wa furaha sana nime enjoy kupita kiasi"  ilikuwa ni sauti ya sarah  msichana wa tatu ambae muda mwingi alikuwa kimya akicheka na kufurahia ucheshi ulio endeshwa na kina baraka.

"Hata mimi nime furahi sana NASHUKURU MWAKA HUU NIMEUMALIZA SALAMA! kuanzia mwanzo wa 2016 mpaka mwisho sija sumbuliwa na homa maradhi wala matatizo yoyote nimevuka mwaka salama thanks god" gadyson aliongea akiwa kwenye furaha.

NAAMU ! gadyson alihesabu kuwa amesha umaliza mwaka 2016 ! ama kweli usio lijua ni usiku wa giza mpenzi msomaji...

Safari ya furaha ilizidi kusonga huku maongezi ya kiucheshi yakitawala ndani ya gari lile..

Wakati baraka anaendelea kuendesha mara ghafla aliutambua muungurumo tofauti kwenye gari yake na hapo akakunja sura akilaani
"Ah chuma kilishaanza kuchemsha acha niweke maji ili ipoe mdogo mdogo" baraka aliongea huku akifunga brek na kuchukua touchi na kushuka nayo akazunguka kwenye mlango wa mizigo akaufungua na kulitafuta dumu la maji lakini hakuliona..
"ujinga huu hili dumu limeenda wapi" aliongea peke yake  huku akizidi kupanga na kupangua mizigo lakini ilikuwa kazi bure...
"wadau  kidumu cha maji tume kitupa wapi" aliwauliza wenzake na wao hawakujua
"kwani wale maafande walikirudisha kweli? maana walikishusha ule muda walipokuwa wana kagua" sarah aliwakumbusha wenzake..
"aah pumbavu zao watakua hawakukipandisha" baraka aliwalaani wale askali wa barabarani... baraka akafunga mlango wa mizigo na kurudi kwenye uskani.
"Hapa ina bidi niendeshe mwendo mdogo mdogo kwani gari inakaribia kuchemsha... ila kilo meta kazaa kutoka hapa kuna sehemu ina mashine ya walter wind hapo kuna kisima tutapata maji" baraka aliongea na wenzake wakaafiki na safari iliendelea kwa mwendo wa speed hamsini.

Kila walipo zidi kutokomea ndipo gari nayo ilizidi kuchemsha na baraka nae akapunguza speed hatimae gari ikawa inatembea taratibu kabisa kana kwamba ilikuwa kwenye foleni za tanzara.

Na mwishoe kabisa gari ile ilizima kabisa na baraka alijaribu kuwasha lakini haikuwaka hata kwa kujaribu...

Wakawa wamekwama katikati ya msitu na hapakuwa mbali sana na lile  pango la goroza!

******--*********;**************

Malikia wa viumbe wale yule mzee kikongwe alikuwa ndani ya pango akisubiria kwa hamu muda ufike na kwenye taswila yake aliwaona jinsi kina baraka walivyo hangaika na gari lao ..!
kikongwe yule aliwasha mshumaa mkubwa uliokuwa pembeni ya sanamu la goroza na kupunguza kiza ndani ya pango..

"Sadaka imefika ..." aliongea na kuanza kutoka nje ya pango lile huku kichwani mwake akiliona lile gari la kina baraka linavyo jikokota kwa mwendo dhaifu...

"Haya muda umefika mbweha mtaenda kuchukua sadaka sita zipo barabarani    ....mzee juma njoo nikuoneshe ukawachukue tuje tufurahie damu zao" malikia kikongwe aliongea baada ya kutoka nje na mzee juma haraka akamsogelea mzee yule..

Kwa hisia na maajabu malikia akamuelekeza mzee juma sehemu waliyo kwama akina baraka.. na mzee juma kwa muujiza mkubwa aliwaona wale marafiki sita waliokuwa ndani ya gari .

"Haya chukua mbweha sita uwaongeze mkalete hiyo zawadi  "  malikia alimuamuru mzee juma...

Wakatoka vijana sita kwenye kile kikundi cha washirikina wakiongozwa na mzee juma wengine wakiwa na mishale  mashoka na wengine mikuki huku wengine mapanga ambayo hutumika na kikosi hiki cha mbweha kukutolea sadaka .
jumla walikuwa saba wakaanza kuondoka kwa kukimbia wakielekea barabarani kuwachukua akina baraka ....huku mioyo yao ikiwa imetawaliwa natamaa ya kumwaga damu...

"gola mchukue diana mrudishe kwao haraka kwanjia ulio itumia kumleta"  mzee yule akamuamuru gola ambae hakupendezwa na amri ile kwani nia na matamanio yake ilikuwa kwa msichana diana usiku wa leo.

Gola akamuinua diana ambae hakuwa na fahamu kabisa akamuweka begani kisha akamtazama mama diana kwa macho ya chuki.
gola akageuka na kutikomea akiwa na diana begani...

"Haya mliobakia anzenu ibada ya kukaribisha sadaka ya usiku huu wa kafara"..... yalikuwa maneno ta malikia.....itaendeleaa...
like na kushare ili kesho iwahi kupostiwa...

RIWATA HII NI SPACIAL KWA MSIMU HUU WA MWAKA MPYA

No comments:

Post a Comment

Iblame my body

RIWAYA   : I'BLAME MY BODY ( NAULAUMU MWILI WANGU ) Imezaminiwa na   Simulizimahiri.blogspot.com Mahakama kubwa ya kesi za jina...