Monday, January 9, 2017

SEHEMU YA TATU

RIWAYA ;ROAD 2017
MTUNZI ;IDDI SIRAJI
WHATS'AAP-0746206428

  Usiku wa kafara..

ilipoishia.....

Gola akamuinua diana ambae hakuwa na fahamu kabisa akamuweka begani kisha akamtazama mama diana kwa macho ya chuki.
gola akageuka na kutikomea akiwa na diana begani...

"Haya mliobakia anzenu ibada ya kukaribisha sadaka ya usiku huu wa kafara"..

endelea..

31December.
Baraka alishuka na kwenda mbele ya gari na kufunua lile bati linayo ifunika injini na hapo macho yake yaka kutana na moshi kutokea kwenye injini.

"Dah gari imechemsha tukisema tuisubiri ipoe inabidi tukae saa zima ....ila kutoka hapa hadi kwenye mashine ya wind walter ni kama dakika kumi na tano hivyo napendelea tukachukue maji huko ili tusichelewe sana"  baraka aliongea huku akiliangalia gari lake lilio fuka moshi...
baraka alikuwa mzoefu wa barabara  hii mara nyingi alishawahi kuitumia na kutembea sana eneo la wind walter

"dah hii ilishakuwa mbaya na mama nilimuahidi nitampigia jioni mpaka sasa hivi saa mbili usiku sijampigia na hapa naona mtandao haukamati" sarah alilaani maana alijua muda ule wazazi wake wanamtafuta kwenye simu...
"Ah usijal chukua tablet yangu  uwa pigie kwa namba yangu ya zantel maana zantel hapa ina kata kwa njia ya satelite" baraka alio ngea kisha akawageukia gadyson na john
"oya wazee wa kazi tufanye maamuzi ya haraka" baraka aliwasihi
"ok kama vipi hawa bibie tuwaache sisi tukachukue hayo maji haraka" john aliongea na muda huo baraka akafungua mlango wa mizigo na kuchukua dumu lisilo na kitu ndani kisha akamsogelea neema.
"sasa jamani tunawaacha humu kwenye  gari sisi tunakuja haraka" baraka aliongea na kumbusu neema kwenye paji la uso(neema na baraka walikuwa na mahusiano ya kimapenzi"

John nae alimsogelea msichana dolla na kumbusu kwenye midomo yake..."kuwa na amani sawa mpenzi" john aliongea baada ya kumpiga busu na dolla alitikisa kichwa kuafiki. ..pia john na dolla walikuwa ni wapenzi

Ni sarah pekee ndie alikuwa msichana asie kuwa na mpenzi kwenye safiri ile yeye mpenzi wake alikuwa akimsubiri kwenye ile hotel walio panga kwenda kushrehekea mwaka mpya pale bagamoyo.

Gadyson nae hakuwa na mpenzi kwenye safari ile ila kuna wakati alijaribu kumchombeza sarah walipo kuwa mbugani mikumi, lakini sarah alionesha msimamo na gadyson akawa kalifutilia mbali lile swala.

Baraka akachomoa ufunguo wa gari yake na kuutia mfukoni akiwa na kidumu aliwasha touch yake yenye mwanga mkali akaaanza kuongoza njia akiwaongoza john na gady kuelekea kwenye maji wakiwaacha wasichana watatu ndani ya gari.

Tayari ilikuwa ni saa mbili usiku na upande wa magharibi mwezi mkubwa wa kuvutia ulikuwa una chomoza.

Kile kikosi cha vijana mbweha kikiongozwa na mzee juma kilikuwa kime wasili eneo lile kwa usiri na  ukimya wa hali ya juu  na wao walikuwa upande wa pili wa barabara na waliwashuhudia akina baraka wakiwaacha wasichana ndani ya gari na wao wakitokomea ndani ya msitu.

"sasa watu watatu wafuateni hao wa kiume sisi tunaenda kuwakamata hao wasichana wao tuna wapeleke kwa goroza" mzee juma aliongea na muda huo vijana watatu wakainuka na kuwafuata kina baraka ...vijana watatu hao walifuata kwa kuwazunguka na kwa mwendo wa ukimya mkubwa.

"dalu wanyatie kimya kimya na wasikuone ukifika jaribu kuufungua mlango wa gari" mzee juma aliongea na kijana dalu akiwa na panga aliondoka akiwa kajikunja kuanzia kiunoni huku aki hama mti hadi mti akihofia ule mwanga wa mbala mwezi usije kumfanya aonekane.

Ilimchukua dakika kumi na mbili  kufika pale kwenye gari ali kokota kokota akiwa anatembele magoti aliufikia mlango na kujaribu kuvuta kile kitasa lakini haukufunguka  akauwacha na kutambaa tena ili akajaribu kufungua mlango wa upande mwingine..

Ndani ya gari wasichana hawakutambua lolote dolla na neema walikuwa wakisikiliza mziki kwenye ear phone na sarah alikuwa busy na tableti akihamisha namba za wazazi wake ili awapigie.....

Baraka na wenzake walitembea kama dakika kumi  kisha akasita kichwani kwake akiwa kuna kitu amekumbuka
"ah nime fanya ujinga ujue humu ni mstuni na kuna wadudu wa na wanyama siku paswa kuiacha bunduki"  baraka aliongea huku akisimama
"ilo nalo neno" gadyson alijibu
"ok ikimbilie sisi tuna kusubiri hapa" john aliongea na baraka akaweka dumu chini akaanza kukimbia kuirudia bunduki yake huku touch yake ikimulika msituni mule  ipasavyo .

Dalu wakati ule ana zunguka ghafla aliona mwanga wa touch kwa mbali ukija kueleke kwenye gari akahamaki na haraka akajua kina baraka wana kuja... haraka dalu akaingi uvunguni mwa gari...

Sarah alijaribu kumpigia  mama yake lakini mama yake alipo pokea simu sarah aliisikia sauti  ya mama yake lakini mama yake hakumsikia sarah..
"dah mtandao una sumbua kweli" sarah alisema na hapo akaona mwanga wa touch ukija upande wao  "oh mara hii wamesha pata maji... ngoja nishuke nimpigie mama huenda nje ya gari nitaongea nae vizuri" sarah aliongea na kutoa lock ya mlango na kushuka akakifuata kisiki cha mti wa mbuyu akakipanda mara moja na kuanza zoezila kumpigia mama yake..

na muda huo baraka nae alikuwa ameisha ifikia gari...

nini kita tokea hapo ?
vipi gadyson na john ? iwapo watatokewa na wale vijana watatu waliotumwa na mzee juma.

like share iendeleee

No comments:

Post a Comment

Iblame my body

RIWAYA   : I'BLAME MY BODY ( NAULAUMU MWILI WANGU ) Imezaminiwa na   Simulizimahiri.blogspot.com Mahakama kubwa ya kesi za jina...