Saturday, October 29, 2016

kisasi

RIWAYA : KISASI
0746206428 whatsapp
imezazaminiwa na simulizimahiri.blogspot.com
Baada ya lile sekeseke zito  lilio sababisha mvutano mkubwa baina ya vyama viwili vya siasa vilivyo minyana vikali vikiwania uongozi wa taifa la tanzania huku kila chama kikipigana kufa kupona ilihali tu kimsimamishe kiongozi kwenye kiti uraisi..
vijembe vya kisiasa pamoja na kukashifiana kwa viongozi walio wania  kiti kile vilichukua  nafasi  kubwa katika sera za kampeni zao, ama hakika uchaguzi huo ulio lindima mwaka 2015 ulikuwa na changa moto kubwa kuliko chaguzi zote zilizopita kwani chama tawala kili pambana na upinzani mkubwa kutoka kwa chama pinzani mpaka kufikia hatua ya kutabiriwa machafuko ya amani katika uchaguzi huo nchini tanzania.
Lakini hakuna mwazo lisilo na mwisho, chama tawala kilishinda kwakishindo na kumsimamisha mgombea wao Mh raisi nakuanza kuiendesha nchi kwa amani na utulivu.
na kama ilivyo kuwa kawaida kila raisi mpya akiapishwa basi hufanya msamaa kwa wafungwa ndivyo hivyo alivyo fanya Mh rais mpya kwa baadhi .
UKONGA ni moja ya magereza yaliyo bahatika kupitiwa na msamaa huo ambao uli wasamehe wafungwa wenye miaka zaidi ya stini na wenye magonjwa makubwa
na siku ya leo ndio walikuwa wakiachiwa..
ndani ya ofisi ya bwana jela asubuhi ya saa tano kulikuwa na wafugwa sita walio kuwa wametawaliwa na furaha kubwa ya kubahatika kupata msamaha wa raisi na muda huu walikuea kwenye usahiri wa kusaini ili waondoke gerezani lile wakaishi maisha yao.wafungwa watano walikuwa ni wanaume ambao kwa haki walikuwa ni mababu kasoro mmoja wao tu ndio hakuonekana kuwa na furaha nae alukuwa ni mwana dada ambaye nywere zake tu zilionesha wazi hakuwa raia harisi wa tanzania japo alikuwa amekonda na kufifia rangi lakini kama ungemuona lazima ungekili kuwa kabla ya hapa huyu dada alikuwa ni mrembo hatari! dada yule hakuwa na shauku kama waliokuwa nayo wale wafungwa wazee yeye alikuwa katulia kabisa nyuma yao akiwa kaegemea ukuta wa ofisi ile..
"haya ni zamu yako dada" aliongea mtu aliekuwa nyuma ya meza ile ya kiofisi na huyu mtu alikuwa ni bwana jela mpya...
yule dada akapiga hatua na kuisogelea ile meza akachukua karamu iliyo kuwa juu ya file lake husika.
"tia sahihi hapa na hapa" yule bwana jela alimuelekeza yule dada
na dada yule akainama kutia sahihi sehemu alizo elekezwa, wakati akitia sahihi ghafla nywere zake alizo zibana kwa nyuma zilifunguka na kuangukia mbele zikilanda usoni kwake mpaka kwenye file alilo kuwa akitia sahihi , yeye akaendelea kutia sahihi kana kwamba hakuziona nywere zake kwamba zimefunguka .
aliachia kwa utulivu ile karamu na kuilaza juu ya file na kuinuka akarudi nyuma hatua huku baadhi ya nywere zikiwa zime landa usoni.
bwana jela alimtazama kwa makini yule dada na kwakuwa bwana jela huyu aliekuwa mpya alimshangaa sana mfungwa yule kwanza  aliona yule dada hakuwa raia halisi wa tanzania asili yake ni Asia pili muonekano wa mwanamke yule alikuwa kama alishawahi kumukona
"wewe unaitwa nani "mkuu wa magereza alimuuliza kwa kumkalipia huku akimtazama kwa makini..
"Mariamu mustapha"  yule mwanamke alijibu kwa sauti iliyo kwaruza ...
"What? ni yule mariamu uliefanya maua.."  mkuu yule mpya wa mageleza alishindwa kumalizia sentesi yake kwa mshangao haraka akachukua file la mariamu lilikuwa na maelezo pamoja na vigezo vilivyo pelekea msamaha wa raisi, akasoma maelezo yale kwa ufasaha.
alishusha pumzi kubwa baada ya kumaliza kusoma kwani maelezo yalikuwa yakidai kumuachia mariamu baada yakutumikia jela miaka sita kwani ndani ya miaka minne mariamu amekuwa akisumbuliwa na kansa ya ini na kupata shinda sana gerezani hivyo mamlaka imependekezwa mariamu aaichiwe huru kwa msamaha wa raisi .
"askari watoe nje ukawakabidhi kwa mtu wa mahakama" mkuu wa magereza hakuwa na la ziada juu ya mariamu cha zaidi alishangaa sana maamuzi ya uongozi kwa kumuachia mariamu alie wahi kufanya mauaji miaka saba iliopita.
wafungwa sita akiwemo mariamu ambao kwa hakika walikuwa huru waliongozwa na askari mpaka nje gereza ambapo kuna gari liliwasubiri ili wapelekwe mahakamani wakapewe hati zao ili warudi uraiani.
Davidi alifurahi sana baada ya kumuona mariamu akitoka katika lango kubwa la jela . kwa furaha isio kifani davidi alupiga ngumi gurudumu la gari alio liegemea
"asante mungu juhudi zangu zimefanikiwa!!!!!" alisema kimoyo moyo davidi!
wakati wakiendelea kusonga kuelekea ilipokuwa imeegesha gari mariamu aligeuka na kulitazama lile jengo la gerezalililo zungukwa na ukuta mkubwa .alilitaza gereza lile huku kumbu kumbu za mateso na shida alizozipata ndani gereza lile zikijirudia kichwani mwake na picha za sura mbali mbali zikipita kichwani mwake ...
machozi yakawa yanamtoka
"Where is my son" aliongea kwa sauti ya kukwaruza  huku kumbu kumbu za siku aliyo nyan'ganywa na kutenganishwa na mwanae mdogo wa kiume ikimrudia  .
"we songa mbele" askari mmoja alimuamuru mariamu huku akimgusa na kirungu begani..
lakini alikuwa kimya
david alipoona hivyo alipiga hatua mpaka alipo kuwa mariamu na kumgusa begani
"upo huru mariamu tuondoke" alisema davidi
"siwezi... kuondoka bila mwanangu wanirudishie mwanangu" mariamu aliongea huku machozi yakimtoka....
HII NI SIMULIZI ITAYO KUJA KWA JINA LA KISASI NI SEHEMU YA PILI YA I BLAME  MY BODY ....0746206428
unaweza kututembelea simulizimahiri.blogspot.com kupata sumulizi nyingine nyingi

Saturday, October 22, 2016

Bonyeza link uisome riwaya hii ya taharuki

Riwaya: The world hates me{dunia ina nichukia)
hali ya mawingu ilitawala katika anga ikiambatana na manyunyu yalio sababishwa na mvua kubwa ilionyesha kwa saa zima iliyopipta, mvua ilionekana kumshtukiza kila mkazi wa mji wa dar es salaam hakuna mtu alieitarajia , mvua hii ilionekana kuwa kero kubwa kwa wakazi wa mtaa wa tandika kwa maana barara nyingi za mataa huo zilijaa mtope yakiambatana namaji. wakazi wachache wa mtaa huo walipitapita wakiwa na miavuli ya o wakielekea madukani na sehemu nyinginezo. maderava wa bodaboda nao waliendelea kupita wakibeba abiria wenye haraka.
Hari ndani ya mtaa watandika haikuonekana kuwa nzuri hata kidogo maana maana polisi walioneka kana kila barabara ya mtaa huo watandika, kila aliye kuwa mkazi waeneo lile alione kushangazwa na uwepo wa polisi hao kwani walionekana kuwa na msako usio kuwa wa kawaida na kila polisi aliku amelowa chepechepe huku bunduki zao zikiwa makini katika mikono yao! Wakazi watandika walizidi kuwa na hofu pale walipo ona gari nne zilizo jaza mapolisi ambao waliruka mmojammoja kutoka kwenye gari na kuigia ndani ya vichochoro vya mtaa huo wa tandika, halikuwa gari moja peke yake bali magari mengi ya police yalindelea kupita kila kona ya mtaa huo wa tandika huku yakiendelea na zoezi hilo la kumwaga police katika vichochoro vya mtaa huo,
hofu ilitanda wakazi wa mtaa huo wa tandika hawa kujua nini kilichokuwa kinaendelea japo baadhi ya watu walibahatisha kwa kusema itakuwa ni oparation ya kusafisha wauza bangi na wauzaji wa madawa ya kulevya, lakin kila mtu alisema la kwake wengiwao waliongea wakiwa kwe vibanda vya chips na wengine wakiwa majumbani mwao wakiwa wamesimama mlangoni na baadhi yao wakiwa vibalazani ,
wakiwa wanaendelea kujiuliza maswali yasiyo kuwa na majibu mara ghafla walishuhudia gari mbili za police zikipita mbele yao zikiwa mwendo mkali zikiwa zimejaza watu waliova nguo za police lakini nguo zao zilikuwa tofauti kidogo, kwa muonekano tu watu waliweza kugundua kwamba ni FFU.!
hofu ikaongezaka !
kabla hawaja tanabahi waliona magari hayo yakiwa mwisho kabisa mwa barara yakifunga brek na kupunguza mwendo na kuanza kukata kona kwa kwa muundo wa kuangaliana kisha madereva wa magari hayao wakakutanisha gari hizo zikawa zime funga barara hiyo, na askali wagari la upande kushoto walionekana kushuka huku wakiwa wameshika vitu kama minyororo, na mmojamoja walianza kushuka huku wakiwa wame tanguliza mbwa wakubwa mbele yao!
kufikia hapo amani ilitoeka kwa wa kazi wa eneo hilo walio kuwa milagoni walifunga milango na kuenda madirashani kuchungulia wakisubiri kuona nini kingetokea, na waliokuwa vibarazani walitafuta nyumba za kuji hifadhi kwa wakati huo ,kuna baadhi walikosa pakwenda wakaamua kutulia walipokuwa wakisubiri tukio ambalo kwa hakika hawakujua ni tukio gani lingetokea kutoka kwa askari wale!
wale askali walioshuka na mbwa walikoki bundiki zao nakuondoka kwa mwendo wa mchamchaka mbwa wao wakiwatangulia kuelekea ndani yamtaa, na askari walibakia kwenye gari la pili wao walishuka nakwenda upande mwingine wa magari hayo kisha wakawa wameangalia upande waliko elekea wanzao wenye mbwa!
mudawote bunduki zao zilikuwa zimekaa makini mikononi mwao.****
kufikia muda huo wa saa 7 police walionekana kila kona ya eneo hilo liliopo karibu kabisa na stend i, kila barabara iliokuwa ina tumika kuingia na kutoka ndani ya stand ya tandika ilifungwa kwa magari ya police na hakuna gari hata moja lilo ruhusiwa kutoka ndani ya stendi hiyo ya tandika!, na watu walipo taka kwenye daradara ili watoke ndani ya stend hyo watembee kwa mguu hawakuruhusiwa na polisi waliokuwa wametanda eneo hilo!
hakuna aliejua kuna nini mpaka kufikia hatua ile!
na wingu yalitanda anga yote ikawa giza na mvua kubwa ikaanza kunyesha.
watu walitawanyika kujikinga na mvua ile, lakini hakuna polisi hata mmoja alie ondoka sehemu alio kuwepo. ****
Mtaani polisi walijaa wakipita huku na huku mvua ikiendelea kuwa nyeshea , polisi wengine waliendelea kusimama sehemu moja ina onekana walia ambiwa wakae sehemu hiyo,
gari moja aina ya rava4 lenye namba za usajili za serekali liingia kwa kasi ya ajabu na kusimama pale kwenye gari ya FFU ilioshusha askali wenye mbwa muda mchache ulio pita, katika gari la rava4 alishuka mwanaume wamakamu alie kuwa amevaa nadhifu nguo za kiraia za heshima, na bila kujali mvua kubwa iliokuwa ikiendelea kunyesha alianza kuelekea kwenye zile gari za FFU na kabla haja zifikia kwenye zile gari askari mmoja alie kuwa hana bunduki lakini alikuwa na bastola kiunoni alionekana kuwa na cheo flani alimkalibia kabla ya fika mtu huyo wa makamu na kumpa heshima kwa kupiga saluti,
"nipe taarifa" alisema mtu wamakamu bila hata salamu!kana kwamba aliona salaamu hiyo haina ummuhimu wakati huo!
" tumefanikiwa kufunga barabara zote zinazo toka na kuingia ndani ya stendi na askari wameenea ndani ya stendi hii.." alijibu askari aliekuwa na bastora kiunoni. mtu wamakamu hakusema kitu ila aliendelea kumuangalia kwa macho yaliyo hitaji taarifa zaidi, na yule askari aliendelea kutoa taarifa....
" ...na ndani ya mtaa tumefanikiwa kufunga barabara si chini ya 12, na askari wame tapakaa karibu robo tatu ya mtaa." askari huyo akawa amesha maliza kutoa taarifa yake, na mtu yule wa makamu aliyevaa nguo za kiraia aliingiza mkono mfukoni na kutoa RADIOCALL, na akabonyeza kitufe flan ,na akaisogeza kalibu ya kinywa chake.
"i.s.p robert naongea" aliongea mtu yule wa makamu.
"report please" sauti upande wapili uliongea.
"tumesha dhibiti upande wa stendi hakuna mtu wala gari litakalo toka nje bila idhini,kwa upande mtaani tumidhibiti karibu robo tatu ya mtaa, nita hitaji kuonana wenyeketi wa mtaa ili watulekeze nyumba za kulala wageni pamoja na vichochoro wanavyo vijua , nita hitaji askali zaidi ili oparesheni ianze" ali maliza i.s.p robert.
"sasa mimi nisha fanya mpago baada ya dakika kumi natano vyombo vyote vya habari vitatangaza juu ya oparesheni ilikuwapa taarifa wakazi watandika ili wawe watulivu wakati opareshen ina endelea, baada ya dakika kumi na nane oparesheni ianze" sauti ya upande wapili uli maliza maelezo.
"ok nime kupata and out" robert aliongea kikakamavu, na akashu mkono wenye radio call na kumgeuka yule askari mwenye bastora kiunoni.
" tuna hitaji mwenyekiti wa eneo hili" alisema robert huku akifuta maji kwenye macho yake alikuwa ameshalowa chapachapa
"hamna tatizo mda mchache uliopita alikuja kuuliza nini kinaendelea, tulimwambia asiondoke ofsin kwake kwa muda huu na alitu onesha ofisi yake ilipo"
"vizuri afande tuma askari wamfuete haraka" alisema na kurudi kwenye gari lake na kuliegemea, dakika kumi badae mwenyeketi wa mtaa aliwasili eneo alilokuwepo robert ****
TAARIFA YA HABIRI YA DHARURA! JAMBAZI ALIYE KUWA AKITAFUTWA MKOANI MWANZA KWA KOSA LA KUUWA POLISI, HUKU AKIHUSISHWA NA MAUJI YA MZAZI WAKE, IMESADIKIKA JAMBA zi HUYO AMEFANIKIWA KUINGIA DAR ES SALAM MTAA WA TANDIKA, TAARIFA ZA HABARI ZINA SEMA YAMETOKEA MAUJI YA WATU WASIO NA HATIA NDANI YA TANDIKA AMBAYO YANASEMEKANA YAME SABISWA NA JAMBAZI HUYO NA KUTOKOMEA NDANI YA YA MTAA WA TANDIKA! POLISI WANA WAOMBA WAKAZI WA ENEO HILO WAWE WATULIVU KIPINDI OPARESHEN IKIENDELEA YA KUMTAFUTA JAMBAZI NDANI YA MTAA HUO MPAKA SASA ASKARI WAMESHAFIKA ENEO LA TUKIO .
radio na tv vyote nchini vili tangaza habari hii ya ghafla kwa upande wa wakazi watandika ni wachache walio isikia maana wakati huo hofu ili tawala mtaa mtaa huo watandika wengi hawa kuwasha vyombo vya habari. ***
mwenyekiti aliwapigia simu wanyekiti wenzake na muda mchache badae walikuwa wamekutana na robert eneo la tukiokila mwenyekiti alieleza mtaa wake ulivyo na nyumba za wageni alizozifahamu katika eneo lake, katika kufuatilia maelezo ya wenyekiti hao, robert na yule askari waliweza kugundua kwamba upande wa magharibi wa mtaa ule ndio eneo pekee ambalo polisi hawa kuwepo kabisa, na upande huo ulionekana kuwa na vichochoro vingi,..
akili na hisia za robert ziliona upande huo wa magharibi huwenda akawa amejihifadhi jambazi waliemtafuta ambae kwa hakika alikuwa tishio, robert alitoa radio call kisha akaisogeza karibu kabisa na kinywa chake
"OPARESHENI IANZE KWA UPANDE WA STENDI KAGUENI KILA GARI FUNGUENI HATA BUTI ZA GARI , NA UPANDE WA MTAANI INGIINE KILA NYUMBA BAR NA GUEST, MSAKO UWENDE KWA KASI KUELEKEA UPANDE WA MAGHARIBI NINA MASHAKA NAPO OVER" alisema robert. "nimekupata sir".
oparesheni ilianza ya kumtafuta jambazi huyo.
baada ya robert kutoa maelekezo taarifa zilisambaa kwa maaskari wote waliokuwa eneo la tukio, namsako ulianza kwa kasi na vurugU kiasi ambacho haikuwahi kutokea, upande wa stend askari waliingia kwenye kila gari lili kuwepo eneo hilo walifungua kila kilicho funguka katika magari hayo , askari wakiwa na picha waliendelea kumuangali kwa makini kila mtu alie kuwa eneo hilo, kuna baadhi ya watu waliwekwa chini ya ulizi walio onekana wamefanana na mtu aliekuwa akitafutwa lakini baada ya kuchunguzwa na kufananishwa ni picha ya mtu huyo waliachiwa, askari waliendelea kutafuta bila kuchoka japokuwa walikuwa wame lowanishwa na mvua iliokuwa ikiendelea kunyesha lakini miili ilikuwa imechemka kwa kuKIMbia huku na kule, stend yote ilikuwa kimya kilicho sikika kwa muda huo ni sauti ya mvua ikiambatana na ngurumo, watu waliokuwepo eneo la stendi walibaki wamesimama pembezoni mwa maduka yaliokuwepo eneo hilo wengine walikuwa wakipigwa mvua wao walikosa pakujikinga na mvua hiyo , polisi baada ya kutafuta sana ndani ya magari waliamua kujigawa wengine waliingia kwenye maduka ya eneo hilo la stendi na watu waliokuwa wame jikinga kwenye maduka wali tolewa nakujiunga na wenzao waliokuwa waki nyeshewa mvua!
*****
robert baada ya kuona msako umeanza yeye alichukuwa askari wanne pamoja na mwenyekiti kwajili ya kumuelekeza eneo la upande wa magharibi, ambapo robert alihisi kuwepo na uwezekano wa mtu aliye kuwa akitafutwa kukimbilia eneo hilo, baada askari wanne pamoja na mwenyekiti kuingia ndani ya gari la robert, gari liliondolewa kwa mwendo usio wakawaida hata kidogo gari liliendeshwa na robert , gari ilikatiza mtaani kwamwendo kasi,
ndani ya gari robert alionekana kuwa na hasira iliyo pitiliza mawazo yake yote yalikuwa ni kumkamata mtu huyo aliekuwa anaanza kuwa tishio nchini, akiwa kama umbali wa hatua stini mbele yake aliona gari lililokuwa katikati ya barabara huku likizungukwa na askari kama wanane ,hapo moyo wake ulilipuka na kuhisi ndani ya gari hilo kutakuwa namtu aliye tafutwa, lakini aliwaona wale polisi hawakuwa na tahadhari hata kidogo maana baadhi yao bunduki zilikuwa zimevaliwa migongoni badala ya kuwa nazo mikononi , hakupunguza mwendo alindelea na speed yake na kuwasogelea askali wale , .
askari walishitushwa na muungurumo wagari na wote wali geuka kwa wakati mmoja walishanga kuiona gari yenye namba za usajili wa serekali, wote walihisi ndani yagari hilo kulikuwa na mkubwa wakazi, wote kijasho kili watoka! na muda huo huo gari ilipiga breki kama hatua tatu mbele kutoka kwa wale askari. na milango yote ilifunguka kwa wakati mmoja na robert alishuka na kutoa bastora yake kiunoni mwake, maaskari alikuwa nao robert ndani ya gari wali weka sawa bunduki zao tayari kwa kuachia risasi, robert alielekeza bastola yake usawa wa gari lile na askari alio kuwa nao ndani yagari walilizunguka gari hilo huku wakielekeza siraha za kwenye gari hilo " NANI YUMO NDANI YA GARI ?" robert ali wauliza wale askari alio wakuta eneo hilo.
* * * *
moses akiwa nyumbani kwake alishangazwa na taarifa ya habari alio kuwa akiendelea kuangalia, macho yake haya kutaka kuamini kwamba jambazi aliekuwa akitafutwa mkoani mwanza sasa yummo ndani ya jiji la dar es salaam. mawazo yake yalikatishwa na mlio wa simu iliyo kuwa mfukoni mwake , aliitoa na kuangalia nani aliekuwa akipiga mara ghafla alikunja uso! kwa sekunde kadhaa alikuwa amesha mtambua mpigaji! alipokea kwa unyonge . " habari afande!" moses aliongea baada ya kupokea.
"uko wapi na sitaki uniambie kwamba uja sikia juu ya tukio linalo endelea tandika" sauti ya upande wapili ilifoka na kumnyong'onyeza moses!
"hapana afande taarifa ndo nimeipata muda sio mrefu" moses aliongea kwa unyonge na hofu,
" baada ya kupata taarifa ukasubiri nikupigiesimu"
"hapana afande"
"sasa sikia mauji yamesha tokea mauaji tangu ABDUL awasili jijini, nenda haraka tandika katika eneo yapotokea mauji kafanye utalatibu wa maiti kupelekwa hospitali? taarifa zote unipe mimi na so mtu mwingine," na simu ikakatwa.
moses alinuka haraka haraka na kuingi chumbani mwake akachukua koti lake jeusi na kulivaa akachukua grove na bastora yake, na kutoka nje bila kuzima tv yake akatoka nje akapanda juu ya pikipiki yenye namba za usajili wa serekari na safari ikaanza.
****
"ndio afande..." alijibu mmoja wa wale askari walioulizwa na robert,
"It's ABDUL!?" robert alimkatisha kabla aja malizia yule askari,
" hapana ila tuna mtilia shaka " askari alijibu kwa kigugumizi!
"kivipi hemu mtoe mlete haraka nje" alisema robert huku akishangazwa na kigugumizi cha yule askari ,
askari mmoja alifungua mlango wagari na kumtoa mzee mweupe mnene, robert alishangaa na hapo aligundua kwamba wale askari walikuwa wanataka rushwa kutoka kwa mzee yule na ndomaana walikuwa wana wasisi mwingi,,ali wageukia wale askari akiwa amekunja uso wake,
"mnamtilia mashaka yapi babu kama huyu mlikuwa mnataka atoe rushwa sio?" aliuliza robert huku aki waangalia mmoja baada ya mwingine.
"hapana afande tusamehe...."alisema yule askari .
"nyie yaani mnaacha kazi muhimu mnaanza kuomba rushwa, au mna ona hii kazi haina umuhimu?" kimya!
"nasema hivi katika hii oparashen nitafukuzisha kazi askari wengi!" alisema huku akirudi ndani ya gari lake na askari wake aliokuwa nao na na mwenyekiti aliekuwa pembeni kidogo walimfuata wakaingia ,
"toeni hilo gari haraka " alisema na baada ya gari kutolewa ali washa gari na kuendelea na safari..
***
kundi la askari kumi na moja wakiwa na gari lao , katika kuulizia ulizia walikutana na kijana aliekuwa na mfuko uliojaa makopo, ni kijana huyu baada ya kudadisiwa na polisi alisema dakika kama kumi zilizopita alikutana na mtu alie onekana kuwa na wasiwasi , polisi mmoja alitoa picha na kumuonesha kijana huyo , kijana alisema ni yeye alie muona aliedakika chache zilizo pita
"...ndio yeye afande lakini ye amevaa miwani ya macho na suti nyeusi, piteni huu uchochoro niliotokea mimi barabara ya tano ndo nilipo kutana nae"alisema kijana huyo muogota makopo huku akielekeza kwa ishara.
askari wali jigawa wanne waliingie kwenye gari hiyo ya polisi, na sita walifuata huo uchochoro, na gari ilindolewa kwa kasi ikizunguka upande wa pili alipokuwepo mtu walie mtafuta.
****
kijana mrefu kiasi mweupe aliekuwa amevaa miwani ya macho mikono yake ikiwa ndani ya mifuko ya koti la suti aliyokuwa ameivaa, na alikuwa amelowa chepechepe, kijana huyo alitembe kwa mwendo wa kasi ajabu, macho yake haya kutilia yale angaza huku na kule alitembea kwa kuchechemea alionekana ku choka sana , alipita kwenye matope bila kujali na ni huyu ndie alie kutana na yule muokota makopo muda mchache uliopita!
****
polisi walio fuata uchochoroni walitembea kwa kasi ya ajabu na kwa umakini wa hari ya juu, ndani ya dakika kumi walikuwa walikuwa wamefikia barabara ya nane ,na kama hatua tisini mbele yao walimuona mtu alikuwa akitembea kwa kasi akisunta mguu mmoja,alikuwa amevaa suti nyeusi waliendelea kumkalibia kwa kasi kubwa huku wakiwa makini asi waone.
****
gari lilo ondoka na askari watano akiwemo dreva lili zunguka mtaa kwa kasi na kuufuata upande walioelekezwa , gari lipopita kama barabara kumi na moja dreva alikata kona na kushika barabara ya kumi na mbili, dreva alikuwa na lengo la dreva ilikuwa kusimamisha gari ili apige simu na kutoa taarifa ili askari waongezwe katika eneo hilo., akiwa mwendo wa kasi mara ghafla mbele yake hatua kama arobaini aliona mtu alievaa suti akiwa anataka kuvuka barara!
****
yule mtu aliekuwa akifuatwa nyuma na askari bila yeye mwenyewe kujua alitembea kwa haraka akisunta ili aivuke barabara alioiona mbele yake, kutokana na waswasi na mawazo pamoja na kelele ya mvua iliyo piga kwenye bati za nyumba za mitaa hiyo, huyo kijana hakusikia kabisa muungurumo wa gari la polisi lilokuwa likija katika barabara aliyokuwa akiiwahi ili avuke,
alipoingia tu barabarani mikono yake ikiwa bado kwenye mifuko wakoti ndipo kwa kihorokikubwa macho yake yaliishuhudia gari ya polisi ikija kwa kasi alipo simama!
haya mtu alie onekana na muogota makopo yupo katikati ya barabara na gari la polisi inakuja kwa kasi alipo simama na polisi wa sita wapo nyuma yake bila yeye kujua je? nini kitatokea?
jina ABDULI TUMEWEZA KULISIKIA MARA MBILI LIKITAJWA JE? ABDUL NI NANI ?
tukutane kesho tupate kugundua mengi zaidi.
Itaendelea...... like na kushare kesho iendelee
MAONI YAKO NIMUHIMU

sophia

simulizi :sophia
mtunzi: iddi siraji
0746206428 WHATSUP
ilipo ishia...
donge zito lika mkaba kooni akashindwa hata kuipokea simu  kilio cha sauti kikataka kumtoka akijikaza na kuya ruhusu machozi yatiririke..
simu ikakata na hapo sophia akapiga hatua kwenda kwenye ule mlango aufungue atoke nje kufanya maamuzi ambayo aliyaona ni sahihi kwake ...
simu ilianza kuita lakini safari hii sophia hakurudi nyuma  alikwenda kuufungua ule mlango wadharula akajitupe
endelea....
alishika kitasa cha mlango ule wa dharula na kukinyonga kwa nguvu  na kuufungua ule mlango lakini hapo hapo alisikia mtu akibisha hodi kwenye mlango ambao ni mahususi kwa ajili ya wodi ile,sophia akawa ametambua kua aliekuwa ana bisha hodi ni muhudu alie kuwa dhamu usiku sophia akawa anajiuliza akamfungulie au atokee mlango wa dharula akafanye maamuzi yake kabla hajaamua cha kufanya macho yake ya liona kitasa cha mlango wa kawaida kikitikisika hapo sophia akajua muhudumu anaingia  ndani ikamlazimu sophia apige hatua za haraka na kurudi kitandani akatoa haraka ile barua kwenye meza na kuirusha uvunguni kisha akajilaza na muda huo simu yake ilikua ina endelea kuita...
milango ya wodi hua haifungwi hivyo muhudumu alivyo gonga mlango bila kuitikiwa ikamlazimu kuingia ndani huku jasho likimtoka !
"hey sophia umelala simu yako inaita" muhudumu huyo aliongea huku macho yake yakionekana kutoka kwenye usingizi wa muda mfupi..
"sophia" aliita tena
"aaaagh ah madamu Glory" sophia aongea akijifanya katoka usingizini
"dada sophia simu yako imeita sana ..." glory aliongea huku akisogea na muda huo simu ikakata kwani iliita kwa muda mrefu..
"ah nilikuwa kwenye usingizi mzito siku isikia" sophia aliongea huku kukata kwa simu ile ikiwa ni ahueni kwake.. glory alisogea na kukaa juu ya meza kumkabili sophia ambae tayari alishainuka na kukaa kitako kitandani pale.
ajabu glory hakuongea kitu ila alimtazama usoni sophia kwa muda!
"dada kuna nini mbona umeniangalia hivyo.." sophia alihoji kwa kushangaa
"sura yako inaonesha ulikuwa unalia  na macho yako hayakuwa kwenye usingizi hata kidogo ..." glory aliongea huku akiendelea kumtizama sophia
"hapana dada kweli nilikuwa nimelala....ulikuwa una fanya nini mbona unajasho dada glory" sophia alihamisha mada
"ngoja nikwambie kweli....
nilikuwa nimeptiwa na usingizi wa muda mfupi lakini nikiwa Karina usingizi nimeijiwa na ndoto mbaya
"ndoto gani dada glory"
"nime ota kuna wodi inawaka moto mkubwa usiozimika na kuna mnyama mkubwa wa aina yake mwenye uwezo wa ajabu akimnyemelea mgonjwa aliekuwemo ndani ya wodi hiyo inayo waka moto " glory akamezamate kisha akaendelea
"lakini ndani ya chumba hicho kuna kengele inapiga mfululizo kisha sauti ya kengele hiyo ikawa inaumiza kichwa changu . nilipo shtuka kutoka usingizini nikasikia chumbani mwako simu yako ikiita kwasauti jasho ndomaana nimekuja kukuamsha jasho likinitoka"
maneno haya yalimshtua sana lakini akajikaza
"ah hapana dada ni ndoto hutu ... ndoto huja mtu anapokuwa na mawazo mengi "
sophia alimzuga glory huku moyoni akijiuliza glory alikuwa mtu wanamna gani
muda huo wakati glory akimtazama alifanikiwa kuona michirizi ya damu kwenye mkono wa sophia na kisha macho ya glory yakaangalia juu kwenye chuma iliyo ning'iniza dripu ambayo bado ilikuwa haija kwisha hii ikamfanya glory ashituke .kama dripu ilikuwa imeisha kwenye  asinge pata mashaka lakini  dripu ilikua haijaisha hii ilimaanisha sophia alichomoa ile dripu na kuna kitu alikusudia kukifanya..
"niambie kwanini umechomoa dripu" glory alimuhoji kwa ukali kidogo huku sura ya glory ikiwa imeanza kubadilika . swali hili lili mshitua sana sophia
"ah doctor aliniambia nikijisikia vibaya niichomoe"
"hakuna daktari mpuuzi wa kukuambia hvyo daktari gani huyo"
"madam Nasra"
sophia alimsigizia nasra ambae hakuwepo muda huo.
na  kabla glory hajauliza uliza tena ghafla upepo ulivuma nje na kwakuwa ule mlango wadharula hakufungwa vizuri na sophia ulifunguka wote wakashtuka na kuangalia na hapo glory akapata kujua kulikuwa kuna kitu cha hatari katika wodi hii usiku huu..
"ah madam nasra kasahau kuufunga huu mlango wa dharula alitumia kutolea maboksi ya dawa kabla hajaondoka"
sophia alionganisha uogo wake na kumshtumu nasra bila kujali
"inamana alitoa kima gendo"
"nafikiri" sophia hakuwa na wasi wasi juu ya kumhujumu nasra kwani yeye binafsi alijua wazi asinge liona jua la siku inayofuata ilikuwa lazima ajiondoe katika ulimwengu usiku ule..
glory aliinuka na kuufunga ule mlango wa dharula huku moyo wake ukiwa umeanza kumshutumu nasra akiamini kweli nasra alitoa maboksi ya dawa kimagendo kupitia mlango wa dharula wa wodi ya sophia , maskini ya mungu glory hakujua kwamba kaongopewa na sophia...
"ok lala sophia kesho tukijaliwa " glory alimuaga sophia na kutoka nje.
Sophia akashusha pumzi huku akaichukua simu yake akaizima asipatikane hewani.kisha akaichukua ile barua akaiweka mezani kwa mara nyingine...
"nisamehe madamu nasra nisamehe glory nisamehe GIKA" alisema sophia
upande wa gika...
wakati yale yote yakiendelea gika alikuwa ndani ya ofisi ya daktari wa magonjwa ya figo usiku ule  akiwa katika maandalizi ya kufanyiwa opareshen!
"kijana wangu gika upo tayari kwa hili tunalo kwenda kufanya usiku huu" daktari mwenye umri wa makamo alimuuliza Gika huku akimtazama kwa kumchunguza
"ndio mzee nipo lidhaa" gika alijibu
"wewe ni kama mwanangu hakuna baba ambae angekubali kumruhusu mwanae wa wa kiume atoe figo yake na ampe mpenzi wake ambaye anatakiwa awekewe figo"
"lakini doctor naamini baba yangu anaweza kutoa figo kwa ajili ya mama iwapo mama atakuwa anaugonjwa wa figo"
"lakini gika sophia sio mke wako na aliwahi kukusaliti" daktari alizidi kumuweka sawa ili gika aachane na wazo la kuitoa figo yake kwa ajili ya sophia alie kuwa taabani akihitaji huduma ya kubadilishwa figo
"kila kosa husamehewa hakuna kosa jipya duniani hapa sophia nilisha msamehe na naya saidia maisha yake kisha tukaanzishe familia bora"
"iwapo utakufa katika oparesheni hii" daktari alimuuliza kwa sauti ya chini
"itakuwa baba amekufa katika harakati za kumsaidia mama..na mama atabaki mzima akisimulia wema wa gika kizazi na kizazi" gika aliamua kumaliza na kumkatisha tamaa daktari juu ya wazo lake la kuzuia
"ok nani atakuwa shahidi wako wa kusaini hii oparesheni hii" daktari ali uliza na kumfanya gika anyongee kwani gika katika hili hakutaka kumshirikisha ndugu ata rafiki mmoja kwa alijua wazi wange mpinga
"ni mimi na wewe doctor ... muonee huruma sophia kama nikuoneavyo mimi usinipinge baba yangu" gika aliongea kwa upole kisha akavuta karatasi ilio kuwa mbele yake na kuitia sahihi yake!
"ok heri mwenye moyo safi.... umekuwa na moyo wa ajabu kijana" daktari aliongea huku nae akiichua ile karatasi akatia sahihi yake na kuibana ile karatasi kwenye file.
"saa saba kamili usiku huu utaingia kwenye chumba cha opareshin mpaka saa tisa opareshen itakuwa tayari kisha itafuatia kwa sophia"  aliongea daktari moyo wa gika ukapata furaha gika akaitazama saa yake ya mkononi..
"bado dakika thelathini na tano.. acha nikapige simu dakika kadhaa" gika alisema
"ok najua unaenda kuogea na sophia...ok maandalizi mema" daktari alisema huku akitabasamu
"gika nae akatabasamu nakutoka nje kwenda nje kupiga simu..
gika alipiga simu lakini hakupokelewa !
(ulikuwa ndo ule muda ambao sophia alikua anataka kufungua mlango wa dharula"
gika akapiga tena lakini hakupokelewa tena...
(ndo ule muda glory alio amka na kumfunguza sophia..)
gika akarudisha simu mfukono na kwenda carteen akisubiri muda wa opsresheni...
saa saba kamili usiku kwa moyo mmoja na upendo wa ajabu gika aliingia kwenye chumba cha oparesheni ambako alikutana na jopo la madakari na bila kupoteza muda oparesheni ilianza..
saa tisa na dakika kumi uparesheni ilikuwa imefanyika na na kundi la wahudumu lilitoka kuelekea ilipokuwa wodi ya sophia ili wampeleke chumba cha oparesheni ili abadilishwe figo awekewe ya gika!
walimkuta glory na kumpa taarifa kwamba wanamchukua sophia akafanyiwe mabadilisho ya figo ..glory alishangaa sana kusikia gika amesha tolewa figo na hapo !
glory akampa file kiongozi wa wahudumu hawa akasaini glory akawaaongoza kwenye wodi ya sophia..
glory aliingia kwenye wodi ya sophia na kumuona sophia akiwa kalala kwenye sakafu!
"dada sophia!" glory aliita huku moyo wake ukipinga
kimya!
glory haraka akamsogelea sophia pale na kumuita huku akimtikisa ...
macho yalimtoka glory baada yakuona kisu sakafuni kikiwa na damu nchani kisha akaona kijeraha kidogo kwenye mkono wa sophia akapeleka sikio lake kifuani mwa sophiaa.....
hapo yowe kubwa likamtoka glory...
sophia hakuwa tena dunia hii alikua kajiua kwa kujikata mshipa mkuu wa damu katika mkono wake wa kushoto.....
itaendelea...
share ili upate mwendelezo

Friday, October 21, 2016

Sophia

mtunzi: iddi siraji
SOPHIA
Bugando mwanza .
Asilimia kubwa ya wagonjwa walikuwa wamisha pitiwa na usingizi huku wengine wakiwa wamejituliza vitandani mwao kana kwamba wamelala lakini walikuwa macho wakiungulia maumivu ya maradhi yao yalio endelea kuwa sumbua  na kuwaweka kwenye hosptali ile ya bugando.
kwa ufupi usiku ule hosptal ilikuwa kimya, pirika za hapa na pale za wahudumu na manesi zikiendelea kwa utulivu mkubwa na ukimya wa hali yajuu..
wodi nambari H 109 ilikuwa ni wodi ya private huku ndani yake akiwemo mgonjwa aliefahamika kwa jina la Sophia .
muda wote usiku ule sophia alikuwa amekaa katika kitanda chake huku mbele yake kukiwa na meza ndogo ikiwa imebeba barua ilio kuwa ikamalizikia kuandikwa na sophia..
sophia aliendelea kuandika ile barua huku machozi yakimtiririka kwa hudhuni kubwa na simanzi ilio kuwa imewaka makazi ndani ya moyo wake.
tayari alikuwa amesha andika ukrasa wa kwanza na sasa alikuwa anamalizia ukrasa wapili na chini kabisa ya barua aliandika kwa maandishi makubwa (GIKA NISAMEHE SANA KWA MAAMUZI NILIYO YACHUKUA) kisha akailaza karamu yake juu ya barua yake  na kwa mkono wake wa kulia akaichumoa sindano ya dripu alio tundikiwa na kufanya damu itiririke kwenye mkono wake kutokea kwenye mshipa aliochomoa ile sindano ,hakuwa na muda wa kuitazama ile damu kwani wakati wake wa kuishi hapa duniani ulikuwa umefikia mwisho kwani sophia alikuwa na maamuzi ya kujiua usiku ule..
"haina maana ya kuendelea kuishi mabaya nilio wahi kumfanyia Gika lakini leo ndio kawa msaada mkubwa katika maisha yangu .. wako wapi? wafanya biashara wenzangu wapo marafiki zangu wa karibu niliokuwa nao katika starehe zote za huu mji wa mwanza  yupo wapi mpenzi wangu nilivuma nae kwenye magazeti kwa skendo za kwa sophia natoka na msanii chipkizi wa mziki wa bongo fleva.. yeye si ndie nilie muona anafaa na kumtelekeza gika nakuamua kumfuata yeye alie nifanya nitambulike kwenye media na magazeti.." aliongea kwa sauti ndogo ilio ambatana na kilio cha chini chini huku nafsi yake ikimsuta kwa mabaya alio mfanyia gika
"ok yote yamepita nikisha pona itanilazimu nikaishi kwa gika kwenye nyumba yake ambayo nilisha wahi kuitukana na kuita ni banda la njiwa huku nikijivunia jumba langu ambalo mpaka sasa imeshapigwa mnanda..
nitamtazama vipi gika nikiwa katika nyumba yake?
na vipi waandishi  wa habari wakini tafuta kwa mahojiano?
hapana siwezi kuishi siwezi kuishi tena"  alisema sophia kupiga hatua emegency door akiwa na lengo la kutoka nje ili ajitupe chini kutoka ghorofha namba 9 aliyo kuwepo .. lakini kabla hajafungua alisikia mlio kutoka kwenye simu yake aliyo iacha kitandani moyo ukamsukuma kuiangalia ile simu na alipo rudi kuiangalia alikuta jina gika kwenye kioo cha simu yake,
gika alikuwa anampigia!
ndoge zito lika mkaba kooni akashindwa hata kuipokea simu  kilio cha sauti kikataka kumtoka akijikaza na kuya ruhusu machozi yatiririke..
simu ikakata na hapo sophia akapiga hatua kwenda kwenye ule mlango aufungue atoke nje kufanya maamuzi ambayo aliyaona ni sahihi kwake ...
simu ilianza kuita lakini safari hii sophia hakurudi nyuma  alikwenda kuufungua ule mlango wadharula akajitupe ......
hii ni simulizi fupi tukutane wakati mwingine tupate kujua hatima ya sophia...

Iblame my body

RIWAYA   : I'BLAME MY BODY ( NAULAUMU MWILI WANGU ) Imezaminiwa na   Simulizimahiri.blogspot.com Mahakama kubwa ya kesi za jina...