Monday, January 9, 2017

SEHEMU YA TATU

RIWAYA ;ROAD 2017
MTUNZI ;IDDI SIRAJI
WHATS'AAP-0746206428

  Usiku wa kafara..

ilipoishia.....

Gola akamuinua diana ambae hakuwa na fahamu kabisa akamuweka begani kisha akamtazama mama diana kwa macho ya chuki.
gola akageuka na kutikomea akiwa na diana begani...

"Haya mliobakia anzenu ibada ya kukaribisha sadaka ya usiku huu wa kafara"..

endelea..

31December.
Baraka alishuka na kwenda mbele ya gari na kufunua lile bati linayo ifunika injini na hapo macho yake yaka kutana na moshi kutokea kwenye injini.

"Dah gari imechemsha tukisema tuisubiri ipoe inabidi tukae saa zima ....ila kutoka hapa hadi kwenye mashine ya wind walter ni kama dakika kumi na tano hivyo napendelea tukachukue maji huko ili tusichelewe sana"  baraka aliongea huku akiliangalia gari lake lilio fuka moshi...
baraka alikuwa mzoefu wa barabara  hii mara nyingi alishawahi kuitumia na kutembea sana eneo la wind walter

"dah hii ilishakuwa mbaya na mama nilimuahidi nitampigia jioni mpaka sasa hivi saa mbili usiku sijampigia na hapa naona mtandao haukamati" sarah alilaani maana alijua muda ule wazazi wake wanamtafuta kwenye simu...
"Ah usijal chukua tablet yangu  uwa pigie kwa namba yangu ya zantel maana zantel hapa ina kata kwa njia ya satelite" baraka alio ngea kisha akawageukia gadyson na john
"oya wazee wa kazi tufanye maamuzi ya haraka" baraka aliwasihi
"ok kama vipi hawa bibie tuwaache sisi tukachukue hayo maji haraka" john aliongea na muda huo baraka akafungua mlango wa mizigo na kuchukua dumu lisilo na kitu ndani kisha akamsogelea neema.
"sasa jamani tunawaacha humu kwenye  gari sisi tunakuja haraka" baraka aliongea na kumbusu neema kwenye paji la uso(neema na baraka walikuwa na mahusiano ya kimapenzi"

John nae alimsogelea msichana dolla na kumbusu kwenye midomo yake..."kuwa na amani sawa mpenzi" john aliongea baada ya kumpiga busu na dolla alitikisa kichwa kuafiki. ..pia john na dolla walikuwa ni wapenzi

Ni sarah pekee ndie alikuwa msichana asie kuwa na mpenzi kwenye safiri ile yeye mpenzi wake alikuwa akimsubiri kwenye ile hotel walio panga kwenda kushrehekea mwaka mpya pale bagamoyo.

Gadyson nae hakuwa na mpenzi kwenye safari ile ila kuna wakati alijaribu kumchombeza sarah walipo kuwa mbugani mikumi, lakini sarah alionesha msimamo na gadyson akawa kalifutilia mbali lile swala.

Baraka akachomoa ufunguo wa gari yake na kuutia mfukoni akiwa na kidumu aliwasha touch yake yenye mwanga mkali akaaanza kuongoza njia akiwaongoza john na gady kuelekea kwenye maji wakiwaacha wasichana watatu ndani ya gari.

Tayari ilikuwa ni saa mbili usiku na upande wa magharibi mwezi mkubwa wa kuvutia ulikuwa una chomoza.

Kile kikosi cha vijana mbweha kikiongozwa na mzee juma kilikuwa kime wasili eneo lile kwa usiri na  ukimya wa hali ya juu  na wao walikuwa upande wa pili wa barabara na waliwashuhudia akina baraka wakiwaacha wasichana ndani ya gari na wao wakitokomea ndani ya msitu.

"sasa watu watatu wafuateni hao wa kiume sisi tunaenda kuwakamata hao wasichana wao tuna wapeleke kwa goroza" mzee juma aliongea na muda huo vijana watatu wakainuka na kuwafuata kina baraka ...vijana watatu hao walifuata kwa kuwazunguka na kwa mwendo wa ukimya mkubwa.

"dalu wanyatie kimya kimya na wasikuone ukifika jaribu kuufungua mlango wa gari" mzee juma aliongea na kijana dalu akiwa na panga aliondoka akiwa kajikunja kuanzia kiunoni huku aki hama mti hadi mti akihofia ule mwanga wa mbala mwezi usije kumfanya aonekane.

Ilimchukua dakika kumi na mbili  kufika pale kwenye gari ali kokota kokota akiwa anatembele magoti aliufikia mlango na kujaribu kuvuta kile kitasa lakini haukufunguka  akauwacha na kutambaa tena ili akajaribu kufungua mlango wa upande mwingine..

Ndani ya gari wasichana hawakutambua lolote dolla na neema walikuwa wakisikiliza mziki kwenye ear phone na sarah alikuwa busy na tableti akihamisha namba za wazazi wake ili awapigie.....

Baraka na wenzake walitembea kama dakika kumi  kisha akasita kichwani kwake akiwa kuna kitu amekumbuka
"ah nime fanya ujinga ujue humu ni mstuni na kuna wadudu wa na wanyama siku paswa kuiacha bunduki"  baraka aliongea huku akisimama
"ilo nalo neno" gadyson alijibu
"ok ikimbilie sisi tuna kusubiri hapa" john aliongea na baraka akaweka dumu chini akaanza kukimbia kuirudia bunduki yake huku touch yake ikimulika msituni mule  ipasavyo .

Dalu wakati ule ana zunguka ghafla aliona mwanga wa touch kwa mbali ukija kueleke kwenye gari akahamaki na haraka akajua kina baraka wana kuja... haraka dalu akaingi uvunguni mwa gari...

Sarah alijaribu kumpigia  mama yake lakini mama yake alipo pokea simu sarah aliisikia sauti  ya mama yake lakini mama yake hakumsikia sarah..
"dah mtandao una sumbua kweli" sarah alisema na hapo akaona mwanga wa touch ukija upande wao  "oh mara hii wamesha pata maji... ngoja nishuke nimpigie mama huenda nje ya gari nitaongea nae vizuri" sarah aliongea na kutoa lock ya mlango na kushuka akakifuata kisiki cha mti wa mbuyu akakipanda mara moja na kuanza zoezila kumpigia mama yake..

na muda huo baraka nae alikuwa ameisha ifikia gari...

nini kita tokea hapo ?
vipi gadyson na john ? iwapo watatokewa na wale vijana watatu waliotumwa na mzee juma.

like share iendeleee

Friday, January 6, 2017

RIWAYA YA ROAD TO 2017

RIWAYA : ROAD TO 2017

SEHEMU YA PILI.

31 DECEMBER.

ILIPO ISHIA..
"Hatuna haja ya kuuana sisi kwa sisi leo usiku mtapata damu ya kutosha na gozola atalizika.... kuna watu wanakuja kupitia ukanda huu leo leo wote sita watakuwa chakula chetu usiku huu" bibi yule kizee aliongea kwa sauti ya juu huku kichwani mwake akiwaona wale watalii wakiendeshwa na baraka....!

"ndio wanakuja kupitia barabara jirani leo tutafurahia damu zao" aliongea tena kwa msisitizo.

Endelea..
USIKU WA KAFARA.

Wote walikuwa kimya hata gola nae hakusema kitu.
"haya kila mtu arudi mahali pake na binti wa mama diana ahifadhiwe mpaka nitakapo rudi kutoka ndani" yule Mzee ali waamulu
"sawa malikia" wote walijibu na kuanza kurudi sehemu waliyo kaa mwazo huku mzee juma akimuhifadhi vizuri yule binti kigoli diana.. na yule malikia kikongwe akarudi tena pangoni aakanene na gunzani.

*****************

Baraka aliendesha gari kwa speed tena kwa umakini mkubwa
"Dah hawa askali wametupotezea muda mwingi sana" baraka aliongea na kuvunja ukimya wa punde
"Ah ila mimi niliogopa sana nilipo muona yule askali katoa bunduki kwenye gari yako " sauti ya msicha mmoja kati ya wale watatu aliongea
"Umeonae dolla ...halafu wewe baraka unatabia mbaya kumbe una bunduki humu muda wote huja tuambia" msichana mwingine alidakia kumuunga mkono msicha dolla namsichana huyu alie dakia aliitwa Neema

"AH vitu vidogo sana kumiliki bunduki kama ile kwangu kama fimbo tu" baraka aliji gamba

"ehee ulisha anza kujisifu mr misifa ...sio ajabu hata hajui kuitumia bunduki yenye" sauti ya kiume kati ya wanaume watatu ndani ya gari ile ili msanifu baraka kwa kumtania

"Umeonaeeh john kaishaanza kujisifu" kijana wa tatu aliimuunga mkono john . nahuyu  aliemuunga mkono john aliitwa   Gadyson huku

wote wakicheka...

Kabla kicheko chao hakijaisha baraka alikanyaga brek ya ghafla kisha wote wakayumba kwa kwenda mbele na kurudishwa nyuma na muda huo baraka akashuka na kwenda kuufungua mlango wa nyuma kabisa kulipo kuwa na mizigo akaipekuwa na kuichukua ile bunduki akarudi nayo kwa wenzake akaingiza mkono mfukoni akatoa mfuniko wa simu akamkabidhi john na kumwambia auinue juu mfuniko ule..

"ENHEEE hivyo hivyo uinuie juu nataka ni ulenge niupige risasi huo mfuniko" baraka aliongea huku akirudi nyuma akawa anaikoki kwa kuvuta kitasa kichoopo juu ya bunduki ile
"ahh acha boya wewe" joh alimaka huku gadyson akitaka kuingia chini ya kiti na muda huo baraka akaanza kuwacheka
"mbona mmeogopa si mmesema sijui kuitumia"  baraka aliongea huku maneno yake yakiambatana na kicheko....muda huo wasichana walikuwa wakicheka kwani wanayajua masihara ya hawa vijana watatu..
"haya tazameni jinsi ya kuitumia " aliongea na wote wakamtazama
"ukitaka kupiga una vuta hiki chuma cha standby kisha hii triger unaibonyeza kwa kidole cha shahada ..." aliongea kisha akageuka akailekezea bunduki mstuni  na kufyatua risasi na mlipuko mkubwa ukasikika pale na wale wote watano waliziba masikio
"HAPPY NEW YEAR"  baraka alilalama kwa sauti ya kusherehekea
"Oya mzee wa manchester tuondoke naona ushaanza sifa zako" gadyson aliongea baraka nae akarudisha ile bunduki huku akicheka
"kumbe wa oga .. " aliongea huku akifungua mlango wa nyuma akaiweka juu ya mizigo akafunga mlango akaingia kwenye uskani..

"Yani huyu jamaa kila kitu chake anacho penda kibaya hilo bunduki lake bovu bovu sauti yake mbaya hata mwizi akija na mshale ana kutagisha... bado timu unayo shabikia mbovu....unavyo penda vyote vibovu kasoro demu wako neema"  john aliendeleza tena utani huku wale mabinti wakicheka
"acha wewe huyo movic ana goli kumi na moja bado mbili amkamate coasta then spurs man city asanal tupo nyuma yao tuna wakimbiza na baiskel lao la miti..nyie acheni timu yangu noma "baraka aliongea huku akianza kuchochea speed

"Ila hawa watu wana masihara sana wamenifanye niwe na furaha sana huu umekuwa mwaka mpya wa furaha sana nime enjoy kupita kiasi"  ilikuwa ni sauti ya sarah  msichana wa tatu ambae muda mwingi alikuwa kimya akicheka na kufurahia ucheshi ulio endeshwa na kina baraka.

"Hata mimi nime furahi sana NASHUKURU MWAKA HUU NIMEUMALIZA SALAMA! kuanzia mwanzo wa 2016 mpaka mwisho sija sumbuliwa na homa maradhi wala matatizo yoyote nimevuka mwaka salama thanks god" gadyson aliongea akiwa kwenye furaha.

NAAMU ! gadyson alihesabu kuwa amesha umaliza mwaka 2016 ! ama kweli usio lijua ni usiku wa giza mpenzi msomaji...

Safari ya furaha ilizidi kusonga huku maongezi ya kiucheshi yakitawala ndani ya gari lile..

Wakati baraka anaendelea kuendesha mara ghafla aliutambua muungurumo tofauti kwenye gari yake na hapo akakunja sura akilaani
"Ah chuma kilishaanza kuchemsha acha niweke maji ili ipoe mdogo mdogo" baraka aliongea huku akifunga brek na kuchukua touchi na kushuka nayo akazunguka kwenye mlango wa mizigo akaufungua na kulitafuta dumu la maji lakini hakuliona..
"ujinga huu hili dumu limeenda wapi" aliongea peke yake  huku akizidi kupanga na kupangua mizigo lakini ilikuwa kazi bure...
"wadau  kidumu cha maji tume kitupa wapi" aliwauliza wenzake na wao hawakujua
"kwani wale maafande walikirudisha kweli? maana walikishusha ule muda walipokuwa wana kagua" sarah aliwakumbusha wenzake..
"aah pumbavu zao watakua hawakukipandisha" baraka aliwalaani wale askali wa barabarani... baraka akafunga mlango wa mizigo na kurudi kwenye uskani.
"Hapa ina bidi niendeshe mwendo mdogo mdogo kwani gari inakaribia kuchemsha... ila kilo meta kazaa kutoka hapa kuna sehemu ina mashine ya walter wind hapo kuna kisima tutapata maji" baraka aliongea na wenzake wakaafiki na safari iliendelea kwa mwendo wa speed hamsini.

Kila walipo zidi kutokomea ndipo gari nayo ilizidi kuchemsha na baraka nae akapunguza speed hatimae gari ikawa inatembea taratibu kabisa kana kwamba ilikuwa kwenye foleni za tanzara.

Na mwishoe kabisa gari ile ilizima kabisa na baraka alijaribu kuwasha lakini haikuwaka hata kwa kujaribu...

Wakawa wamekwama katikati ya msitu na hapakuwa mbali sana na lile  pango la goroza!

******--*********;**************

Malikia wa viumbe wale yule mzee kikongwe alikuwa ndani ya pango akisubiria kwa hamu muda ufike na kwenye taswila yake aliwaona jinsi kina baraka walivyo hangaika na gari lao ..!
kikongwe yule aliwasha mshumaa mkubwa uliokuwa pembeni ya sanamu la goroza na kupunguza kiza ndani ya pango..

"Sadaka imefika ..." aliongea na kuanza kutoka nje ya pango lile huku kichwani mwake akiliona lile gari la kina baraka linavyo jikokota kwa mwendo dhaifu...

"Haya muda umefika mbweha mtaenda kuchukua sadaka sita zipo barabarani    ....mzee juma njoo nikuoneshe ukawachukue tuje tufurahie damu zao" malikia kikongwe aliongea baada ya kutoka nje na mzee juma haraka akamsogelea mzee yule..

Kwa hisia na maajabu malikia akamuelekeza mzee juma sehemu waliyo kwama akina baraka.. na mzee juma kwa muujiza mkubwa aliwaona wale marafiki sita waliokuwa ndani ya gari .

"Haya chukua mbweha sita uwaongeze mkalete hiyo zawadi  "  malikia alimuamuru mzee juma...

Wakatoka vijana sita kwenye kile kikundi cha washirikina wakiongozwa na mzee juma wengine wakiwa na mishale  mashoka na wengine mikuki huku wengine mapanga ambayo hutumika na kikosi hiki cha mbweha kukutolea sadaka .
jumla walikuwa saba wakaanza kuondoka kwa kukimbia wakielekea barabarani kuwachukua akina baraka ....huku mioyo yao ikiwa imetawaliwa natamaa ya kumwaga damu...

"gola mchukue diana mrudishe kwao haraka kwanjia ulio itumia kumleta"  mzee yule akamuamuru gola ambae hakupendezwa na amri ile kwani nia na matamanio yake ilikuwa kwa msichana diana usiku wa leo.

Gola akamuinua diana ambae hakuwa na fahamu kabisa akamuweka begani kisha akamtazama mama diana kwa macho ya chuki.
gola akageuka na kutikomea akiwa na diana begani...

"Haya mliobakia anzenu ibada ya kukaribisha sadaka ya usiku huu wa kafara"..... yalikuwa maneno ta malikia.....itaendeleaa...
like na kushare ili kesho iwahi kupostiwa...

RIWATA HII NI SPACIAL KWA MSIMU HUU WA MWAKA MPYA

PENZI LA FUKARA

RIWAYA PENZI LA FUKARA MATESO

MTUNZI : ZUBERI MARUMA

WHATSUP : 0652281153

CHAPISHO NO 01

(FUMBO LILILOFUMBWA)

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI

Kila ninapojaribu kufumba macho yangu nikusahau uwa nashindwa.

Siuamin moyo wangu kama kweli ipo  siku ungeniacha

Tena katika kipindi ambacho nakuitaji zaidi.kipindi ambacho ndo ningetakiwa nile  matunda ya masomo yako

Leo hii Mimi na wewe tumekuwa kama paka na panya

Lazima nilipize kwa ulilolitenda?!

                   ************

Uso  wake ulikunjamana kwa hasira,mapigo yake ya moyo yaliongezeka kila muda ulipokuwa ukipotea,

Akalifungua kabati lililokuwa Mbele ya macho yake na kupeleka mkono ndani ya kabati lile,akawa anatafuta kitu katikati ya nguo

Akakipata

Ilikuwa ni bastola ndogo,akaiangalia kwa sekunde kadhaa na kuipachika kibindoni

Akalifunga vizuri kabati lile

Hakika moyo wake ulijaa majonzi,simanzi
,sononeko,maumivu tele yaliushambulia moyo wake....

kama kulia alishalia sana mpaka machozi yakamkauka!

maumivu makali yalikishambulia kichwa chake! yamkini ni kutokana na msongo wa mawazo ama kitendo chake ya kulia sana.....

kulilia mapenzi.

Akalifata droo lake akalifungua na kutoka na kalamu na karatasi akakaa katika meza na kuanza kuiandika barua,

huku machozi mepesi yakiloanisha mashavu yake na baadhi ya matone yakiangukia karatasi lile...

barua ile aliianza kwa kuiandika hivi:

"Kwako mpenzi SHONAIZAR!,

najua u mzima wa afya!,mimi kifikra sipo vizuri!
sidhani kama utaniuliza kwa nini!

sababu nadhani waijua

ila tambua kama mapenzi ni hisia!, hisia zangu zilikuwa kwako , uliniteka kifikra sikutaka nichomoke moyoni mwako, ulinifanya mfungwa katikati ya moyo wako, sikuona mwanamke kwa uzuri afikiaye umbo lako...

Ulitumia udhaifu huo kuntesa mwenzako, ni ahadi ngapi ulini ahidi kwamba utonisaliti?!, ni mara ngapi ulinambia kwamba UNANIPENDA sana?!,

kumbe wewe ni mwanahizaya ulojaa unafki eeh!?!...au kisa mimi ni fukara?,au kisa sina pesa?!

shone penzi langu kwa gharama yoyote lazima litalipwa!, machozi yangu niyatoayo kwa sababu yako yatakugarimu my x!,

tambua kama uliunyakua moyo wangu kwa kuni adaa kwamba unanipenda,

malipo yako nitakunyanganya roho yako,...

leo nayachukia mapenzi

kumbuka wewe ndo ulinifanya niyapende!

nakumbuka kipindi kile kwa mara ya kwanza tulipo onana, ndo kwanza ulitoka masomoni TABORA GARLS na kuja kijijini kwetu kufanya utafiti wa mimea na majani ukiwa na wenzako

mimi nikiwa mchungaji wa Mbuzi ndo kazi nlostaili kwa kipindi kile.

mbona marafiki zako wote walikukimbia pale nyoka mwenye sumu kali alipokugonga?

ZUBERI nikajitolea SHONAIZAR kukusaidia!

kosa langu lipo wapi hapo?

najuta kukufahamu

CHOZI LANGU LAZIMA LILIPWE

niliamua kukuchukua mpaka nyumbani kwangu nilipo kuwa naishi peke yangu

nikaanza kuku hudumia kwa madawa asili mpaka ukapona....

Malipo yangu yalikuwa nin?!
kama si kufungwa?

ulishindwa kunsaidia pale marafiki zako walipokuja na wazazi wako wakanikamata heti nimekuteka!!

msaada wangu ukawa adhabu kwangu ,kwa mara ya kwanza mchunga mbuzi kutoka kijijini nikaingia mjini nikiwa chini ya ulinzi mkali!

nyumbani kwangu pakawa segerea!

yani ung'atwe na nyoka nkuchukue nkutibu nionekane nlikuteka?! ila yote nilivumilia,

ulikuja kuniangalia!

na dhamana ukanitolea!, ukisema wazi kwamba mimi ndiye niliyekusaidia! nadiriki kusema msaada wako ndo ulikuwa huo kwangu!

mpz nishkuru kwa ilo!

kwa kunitoa mahabusu na kunitafutia kazi DAR!

sawa pengine labda kwa kuwa sikujua lengo lako mpaka pale ulipontamkia kwamba UNANIPENDA wewe ndo ulinambia siyo mimi niliyekutamkia!.

.kama kweli ulikuwa unanipenda iweje leo hii uje unsaliti?! utamu wa penzi lako ugeuke shubiri kwangu?

naapa my! lazima penzi langu utalilipa!...

hata ikibidi kwa ncha ya upanga!

ila sitokuacha mzima ama zangu ama zako!

SHONE mpenzi kumbuka!!!.....

nilikukubali kwa kuwa u! mwanamke mrembo,mwenye wajihi wa "black beuty" na macho malegevu kama unasinzia!,

dimpozi mashavuni, ulijaliwa miguu minene ya bia!, ni vigumu kwa mwanaume kukataa ombi lako!...

ni mara ngapi ulililia kifuani kwangu?, 

ukinielezea jinsi unavyonyanyasika kwenu?! kisaa.....

hata ulivyonielezea stori yako ya maisha, iliniuma mpenzi sikusita kulia kwamba mama yako alishafariki na sasa unaishi na mama wa kambo, 

anayekunyanyasa kwa masimango bila huruma kukupatia!  sikuweza kuzuia machozi kunitoka!

shetani mkubwa wewe!

nilikulilia nikikuonea huruma kwa nini nisingekuacha ukateseka? nakuchukia wewe mwanamke! nawachukia wanawake wote.....

sababu ikiwa ni wewe kahaba mmoja!

nitaridhika nitakapo ugawanya ubongo wako! kwa furaha sitosita kuula kwa ukatili ulontendea nipo tayari kufungwa,nipo tayari kunyongwa,pindi nikisababisha mauti yako....

KWA NINI KIJANA HUYU ANA HASIRA HIVI KIPI KIPO NYUMA YA PAZIA ITAENDELEA

UKITAKA VIPANDE VYA MBELE VYA RIWAYA HII JIUNGE NA GRP LA MALIPO WHATSUPP 1500 KWA MWEZI PATA VIPANDE 20 KWA 1000

Iblame my body

RIWAYA   : I'BLAME MY BODY ( NAULAUMU MWILI WANGU ) Imezaminiwa na   Simulizimahiri.blogspot.com Mahakama kubwa ya kesi za jina...